SIKU YA UZAZI MZUNGUKO WA KAWAIDA NA MREFU SIKU 28-35
****NOTE, KAMA HUJUI KUHESABU SIKU ZA MZUNGUKO WAKO BASI TAFUTA MAKALA IPO HAPA CHINI
》》》》》
Kwa wale wanandoa wenye uhakika na MIZUNGUKO YAO ya mwezi. Mfano una uhakika kabisa ya kwamba mzunguko wako wa hedhi ni siku 28 au 32 au 35 na kwamba mzunguko huu umeuona kwa muda wa miezi mitatu basi leo nawapa SIRI YENYE UHAKIKA WA 70% kujua siku zako za uzazi.
MZUNGUKO WA SIKU 28 KWA MFANO
SIKU YA 14 NDIO SIKU YA UZAZI.
FORMULA IKO HIVI
>>>>hesabu siku 15 kuanzia siku ya 28 na kurudi nyuma, yaani tarehe 28 siku ya 1, tarehe27 ya pili,26 ya tatu,25 ya nne ,24 ya tano,23 ya sita,22,21,20,19,18,17,16,15, na tarehe 14 ni siku ya kumi na tano
Katika mzunguko huu siku nzuri ya kuanza kuwa karibu na mwenzako ni kuanzia siku ya 12 hadi siku ya 16.
Mfano huu ni kwamba kama umepata bleed tarehe 1 mwezi wa 7 na mzunguko wako ni siku 28 basi tarehe 14 ndio SIKU YA UZAZI, lakini wewe anza shughuli tarehe 12 hadi 16. Hii ni kwa sababu yai likitoka katika nyumba yake ya mayai linaweza ishi masaa24 tu wakati mbegu za kiume zinaweza ishi masaa hadi 72 na zaidi
MZUNGUKO WA SIKU 34 KWA MFANO
SIKU YA 20 NDIO SIKU YA UZAZI
FORMULA IKO HIVI
Hakikisha mzunguko huu ni mzunguko ulioupata katika miezi mitatu iliyopita. Kama mzunguko unarukaruka basi formula hii haiwezi kukufaa.
Mfano Umepata hedhi mwezi wa saba tarehe 1 manayake siku ya 34 ni mwezi wa 8 tarehe 3. Sasa hesabu siku 15 kuanzia tarehe 3 mwezi wa 8 na kurudi nyuma.
Yaani tarehe 3 mwezi wa 8 itakuwa siku ya kwanza ,tarehe 2 mwezi wa 8 itakuwa siku ya 2,tarehe 1 mwezi wa nane itakuwa siku ya 3 ,tarehe 31 mwezi wa 7 itakuwa siku ya 4, tarehe 30 siku ya 5, endelea 29,28,27,26,25,24,23,22,21, hadi tarehe 20 itakuwa siku ya 15.
>>>Katika mfano huu ni kuwa kama umepata bleed tarehe 1 mwezi wa 7 basi SIKU YAKO YA UZAZI ni tarehe 20. Kwa hiyo unatakiwa kuwa karibu na mwenzio kuanzia tarehe 18 hadi 22.
USHAURI WA BURE ni kwamba katika siku hizi Epuka kuwa mgomvi na mnyimi kuwa mkarimu na mpole ili uongeze furaha ya mwenzako afanye kazi kwa bidii na vizuri.
Sasa tarehe zinaambatana pia na dalili moja kubwa ya kuwa na UTEUTE UKENI, ute huu ni ule kama utaingiza vidole viwili katika uke na kisha ukitoa vitanue kama unaweka alama ya V. UTAONA UTE UNAOVUTIKA KAMA UZI.
BASI JUA KWA HAKIKA HIYO NDIYO SIKU YAKO YA UZAZI. Kama utajaribu miezi kadhaa na kukosa kushika mimba basi tambua ya kwamba kuna tatizo lingine kubwa ama kwa mwenzako au kwa wewe mwenyewe.
>>>> IKIWA UNA MATATIZO YA BLEED AU HEDHI YENYE KURUKA RUKA AU HAIPO KABISA AU UNATOA DAMU NYINGI AU INAKAA MUDA MREFU ZAIDI YA SIKU 7 AU NI ILE INATOKA SIKU MOJA TU BASI USISITE KUWASILIANA NASI KWA USHAURI ZAIDI <<<<<
PI UNAKARIBISHWA KUNUNUA PEDI ZETU ZENYE DAWA NA ZENYE UWEZO WA KUTIBU MIWASHO, FANGASI NA MAUMIVU WAKATI WA SIKU ZA HEDHI
Call/txt 0767925000
Watsap 0622925000
Friday, 8 July 2016
ITAMBUE SIKU YAKO YA UZAZI
Sunday, 22 May 2016
ZIJUE TABIA 10 ZINAZOHARIBU FIGO
By Masha Masanja
Call/txt/whatsapp 0622925000
Kwa kifupi sana leo tunakutajia baadhi ya Tabia zinazochangia kuharibika kwa Figo. Tutambue kuwa tatizo hili la kufeli kwa figo limeshawakumba wengi na baadhi yao wameshapoteza maisha.
Ukiwa mzima mshukuru Mungu na ni vyema ukasoma makala hii ili kujinusuru na janga hili la kuharibikiwa figo.
Hizi hapa ni baadhi ya tabia 10 zinazoharibu figo:
1. Kubana mkojo kwa muda mrefu
2. Kutokunywa maji ya kutosha
3. Kutumia chumvi nyingi
4. Kula nyama mara nyingi zaidi
5. Kutokula chakula cha kutosha
6. Kuchelewa kujitibu maambukizi madogomadogo
7. Kutumia visivyo dawa za maumivu
8. Utumiaji wa madawa kwa ajili ya Insulin
9. Kunywa pombe kupita kiasi
10. Kutopata muda wa kutosha kupumzika
Tafadhari share makala hii kwa watu wengi zaidi ili nao wapate kujifunza na kisha kujinusuru na tatizo hili.
whatsapp 0622925000
Tuesday, 19 April 2016
JINSI YA KUIMARISHA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA KIRUTUBISHO KILICHOTOKANA NA NYANYA
Ni mara nyingi tumekuwa tukizungumza kuhusiana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume chanzo chake pamoja na mambo ya kufanya ili kulimaliza tatizo hilo.
Katika makala zilizopita niliongelea baadhi ya mambo yanayoweza kuchangia kuwa na tatizo hilo. Tembelea www.shinyangabusiness. blogspot.com ili kuyajua mambo hayo ambayo ni pamoja na ulevi, utumiaji wa dawa za kusisimua nguvu za kiume (vega) na upigaji sugu wa punyeto.
Sasa tuone jinsi kirutubisho kilichotengenezwa kutokana na nyanya aina ya Lycopene ambazo hulimwa nchini Thailand kinavyoweza kuwa msaada katika kutibu tatizo hili la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi (mwezi mmoja hadi mitatu).
Kirutubisho hiki ni aina ya nyanya zilimwazo nchini Thailand ambacho baada ya utafiti wa muda mrefu imedhihirika kuwa kina uwezo mkubwa wa kuboresha uzalishwaji wa mbegu za kiume hivyo kuweza kuwasaidia hata wanaume wenye matatizo ya uzazi au kutozalisha.
Kwa kitendo hicho ina maana kirutubisho hiki kinaimarisha misuli ya uume iliyolegea kutokana na upigaji wa punyeto ambapo ndiyo chanzo kikubwa cha wanaume wengi kuwahi kumaliza (kupizi mapema chini ya dakika 3) wakati wa tendo la ndoa.
Mmea huu wa nyanya sasa umeboreshwa zaidi na unapatikana katika mfumo wa vidonge (capsules) na unaweza kujipatia popote ulipo Tanzania. Maana kama ungebaki katika mfumo wa nyanya ingekuwa ngumu kusafirisha aina hiyo ya nyanya kutoka Thailand hadi barani kwetu Afrika.
Mbali na kusaidia katika masuala ya uzazi, vidonge hivi husaidia pia matatizo mengine kama Presha ya kupanda, kansa ya matiti, macho, vidonda vya tumbo, matatizo ya moyo na Asthma.
Kwa wanaume inashauriwa kutumia kirutubisho hiki angalau mara 2 hadi 3 kwa mwaka ili kujikinga na kansa ya TEZI DUME.
Matumizi yake unameza kidonge kimoja asubuhi na jioni pia kimoja.
Waweza jipatia vidonge hivi visivyo na kemikali katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Tanga, Morogoro, Mbeya, Zanzibar na Dar as salaam. Mikoa mingine mnaweza kutumiwa kupitia ofisi za Mabasi
Mawasiliano
0622925000(whatsapp)
0767925000
0784925000
Monday, 11 April 2016
MATIBABU YA MIFUPA, KIUNO, MGONGO NA MACHO YALIYOATHIRIWA NA KISUKARI
KAMA UNA MATATIZO YA MIFUPA, KIUNO, MGONGO, MATATIZO YA MACHO YALIYOATHIRIKA KUTOKANA NA KISUKARI BASI TIBA HII HAPA
Shark cartilage is a dietary supplement made from the dried and powdered cartilage of a shark; that is, from the tough material that composes a shark's skeleton.
Shark cartilage (tough elastic tissue that provides support, much as bone does) used for medicine comes primarily from sharks caught in the Pacific Ocean. Several types of extracts are made from shark cartilage including squalamine lactate, AE-941, and U-995.
Shark cartilage is most famously used for cancer, including a type of cancer called Kaposi’s sarcoma, that is more common in people with HIV infection. Shark cartilage is also used for arthritis, psoriasis, wound healing, damage to the retina of the eye due to diabetes, and inflammation of the intestine (enteritis).
Some people apply shark cartilage directly to the skin for arthritis and psoriasis.
FOR MORE DETAILS PLEASE CALL US ON 0767925000 OR WHATSAPP 0622925000.
TUTAKUTUMIA POPOTE ULIPO...!
Friday, 8 April 2016
ANGALIA VYAKULA HIVI VINAVYOIMARISHA VIUNGO VYA UZAZI VYA MWANAUME
VYAKULA HIVI VI 4 VITAKUSAIDIA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME.
Kichocheo cha testosterone au kwa Kiswahili , japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume.
.KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA, KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI.
NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE?
Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3, vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhiwakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wetu tunakosa vitamini D kwa sababu muda mwingi tunautumia tukiwa ndani tukiendelea na shughuli zetu. Zinc ni madini muhimu ambayo hupatikana kwenye baadhi ya vyakula.
NINI HASA KINASABABISHA KUPUNGUA KWA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE KWENYE DAMU
Mawazo au stress ni muuaji asili wa kichocheo cha testerone, pale unapokuwa na stress basi Tezi ya Adrenal hutengeneza kichocheo iitwayo Cortisol ambayo inapoenda kwenye damu hupunguza ufanyaji kazi wa kichocheo cha kiume cha testosterone ndani ya mwili. Hivyo kama unataka kuepusha tatizo hili ni wazi kwamba unahitaji kupuza stress na kiwango cha cortisol.
AINA ZA VYAKULA AMBAVYO HUSAIDIA KUONGEZA UZALISHAJI WA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE
Ijapokuwa kuna njia nyingi za kusaidia kuongeza kiwango cha kichocheo cha kiume au Testosterone, uzalishaji wa kichocheo hii unategemea zaidi upatikanaji wa viini lishe fulani ambavyo vinapatikana ndani ya vyakula tunavyotumia.
1. KOMAMANGA (POMEGRANATE)
Tunda hili zuri lenye rangi nyekundu likiwa limeiva limekuwa likitumika kama dawa kwa karne nyingi sasa. Kutokana na uwezo wake mkubwa kama kiondoa sumu (antioxidant), pia upatikanaji wa vitamini A,C, E na madini ya chuma, tafiti za kisayansi zinasema kuwa unywaji wa glass 1 ya juisi kwa siku itokanayo na matunda haya inaongeza kwa asilimia 16 mpaka 30 ya hamasa ya tendo la ndoa. Lakini pia inashauriwa zaidi kula tunda lenyewe ili kwanza kufaidi nyuzinyuzi (fiber) ambazo zina umuhimu kiafya pia itakusaidia kutokula kiwango kikubwa cha sukari kilichopo kwenye matunda.
2. MAFUTA YA MIZEITUNI
Mafuta ya mizeituni yana uwezo mkubwa sana wa kuongeza kiwango cha kichocheo cha Testesterone kinachozalishwa na mwili. Tafiti zinasema watu wanaotumia mafuta ya mizeituni kila siku,kiwango cha testosterone huongezeka kwa asilimia 17 mpaka 19 ndani ya week.
3. NAZI
Mwili unahitaji mafuta mazuri ili kuengeneza kichocheo nyingi, ikiwemo kichocheo cha testosterone. Nazi zinasaidia mwili kutengeneza mafuta mazuri ambayo yanahitajika na mwili, pia mafuta yanayopatikana kwenye nazi husaidia mwili kuwa na uzito mzuri na pia kupunguza mafuta mabaya yasiyohitajika na mwili na hivyo utagundua kuwa kurekebishwa kwa uzito wa mwili basi kunasaidia uzalishaji wa kichocheo cha kiume na utakubaliana nami kuwa uzito mkubwa ni chanzo cha tatzo la upungufu wa nguvu za kiume kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa kichocheo cha kiume.
4. MBOGA ZA MAJANI
Mboga za broccoli na cauliflower zinasaidia mwili wa binadamu kutoa kiwango cha kichocheo cha estrogen kilichozidi ndani ya mwili na hivyo kuongeza kiwango cha testosterone ndani ya seli
5. PROTINI ITOKANAYO NA MAZIWA
Protini hii ambayo hupatikana kwenye sehem ya maji ya maziwa inazuia mwili kutengeneza kias kikukwa cha kichocheo cha cortisol na hivyo kuongeza uzalishwaji na ufanyaji kazi wa wa kichocheo cha Testosterone, hapa ielewele kwamba kichocheo hizi mbili huwa zinapishana moja ikiwa nyingi kwenye damu basi ingine huwepo kwa kias kidogo kwenye damu.
DALILI ZIFUATAZO ZINAONESHA KWAMBA UNA UPUNGUFU WA KIWANGO CHA TESTOSTERONE
• Mwili kukosa nguvu mara kwa mara
• Upungufu wa nguvu za kiume
• Kupungua kwa hamasa ya tendo la ndoa
• Kuongezeka uzito kupita kiasi
• Shinikizo la damu kupanda
• Kupungua kwa uwezo wa misuli kufanya kazi
NJIA ZIFUATAZO ZITASAIDIA KUONGEZA KIWANGO CHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE
1. MAZOEZI YA MWILI
Kupunguza uzito usiohitajika na mwili ni njia mojawapo asilia ya kuongeza kiwango cha kichocheo cha kiume.
2. PUNGUZA KIWANGO CHA MSONGO WA MAWAZO
Mwili Unapokuwa na msongo wa mawazo basi hupelekea uzalishaji kwa wingi wa homoni iitwayo cortsol ili kupamban na hali hiyo, lakini uoande wa pili ni kwamba kiwango kikubwa cha cortsol kwenye damu hupelekea ufanyaji kazi ya homoni ya kiume yaani testosterone kupungua
3. PUNGUZA MATUMIZI MAKUBWA YA VYAKULA VYENYE SUKARI NA WANGA
Matumizi makubwa ya vyakula vyenye wanga na sukari hupelekea mwili kutengezeza kiwango kikubwa cha homoni ya insuini ili kubadilisha kiwango hcho cha sukari na kukihifadhi kama mafuta, hivo mpenzi msomaji tambua kwamba kadiri unakula wanga na sukari nyingi ndipo kias kikubwa cha insulini kinavomwagwa kwenye damu na ndivyo ufanini na utolewaji wa homoni ya kiume unavopungua.
TEZI DUME NI NINI?? Na UHUSIANO ULIOPO KATI YA TEZI DUME NA UZALISHAJI WA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE
TEZI DUME NI NINI
Hii ni tezi (kokwa) ambayo inapatikana katika mfumo wa uzazi wa mwanaume katika shingo ya kibofu cha mkojo. Kazi yake kubwa ni kutengeneza maji maji ya uzazi kwa mwanaume(shahawa) ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizotengenezwa kutoka kwenye korodani na husaidia kusafirisha mbegu za kiume na kuzifanya zibaki hai kwa muda unaostahili. Kikawaida wanawake wana kiwango kidogo sana cha kichocheo cha testosterone kwa maisha yao yote
Tezi hii huwa inaongezeka uzito au ukubwa kadri umri wako unavyozidi kukua. Na nimekwambia kuwa tezi hii ipo katika shingo ya kibofu cha mkojo na hivyo basi ukuaji wake unaweza kuathiri mfumo mzima wa utoaji mkojo kwenye kibofu(Incomplete bladder emptying) .
Tafiti zinaonesha kwamba tezi huanza kuongezeka uzito kuanzia miaka 25, na huendelea kukua kila siku kadri umri unavyo enda. Kuongezeka kwa uzito wa tezi yako ya kiume sio tatizo kimatibabu kwani kipimo cha kuonesha moja kwa moja umefikia hatua sio nzuri ni pale unapoanza kupata dalili zenye kuzuia mkojo kutotoka vizuri (obstructive symptoms). Hivyo uzuri ni kwamba kuanzia pale tezi inapokuwa inaongezeka ukubwa hadi kufikia kuonesha dalili mbaya ni hadi unapofikia angalau umri wa miaka 60 na kuendelea , pia inaweza hata ikatokea hata unapokuwa una umri chini ya miaka 50 inategemea na mwili wako kibaolojia. Basi kukua huku kwa tezi bila sababu ya msingi tunaweza tukawa na hitimisho la magonjwa makuu mawili au matatu,Kwanza Benign Prostate Hypertrophy (BPH) aka Kukua kwa tezi dume, pili Prostate cancer Hii ni kansa ya tezi dume na Tatu Uvimbe kwenye kibofu cha mkojo.
Tafiti zinasema kwamba tatzo la Tezi dume linaweza kuziwa kutokea kwa njia za nje, yaani namnisha kwa kutumia ama kula vyakula fulani fulani, kiwango kikubwa cha kiini lishe kiitwacho lycopene husaidia kuondoa uwezekano wa mtu kuugua tezi dume. Lycopene hupatina akwenye matunda yanya. Hapa mpenzi msomaji unaweza kujiuliza kama tunatumia nyanya kila siku kwenye mboga je iweje tuugue tatizo la tezi dume?? Jibu ni kwamba kiasi kidogo sana cha lycopene hufonzwa na mwili kutoka kwenye matunda ya nyanya tunayokula hivo inahitaji ule mamia ya nyanya kila siku ili kufidia hilo gepu.
LAKINI KAMA TAYARI UMESHAPATA TATZO LA KUKUA KWA TEZI DUME BASI TUMEFANIKIWA KUTENGENEZA KIRUTUBISHO KUTOKANA NA NYANYA, kitasaidia kupenya ndani ya tezi dume, kuua bacteria na pia kukarabati sehem zilizoathiriwa na bacteria na hivyo kuzuia kutokea kwa saratani ya tezi dume.
Kirutubisho hiki kina vidonge 30 na unatumia vidonge viwili mara mbili kwa siku. Kwa maoni ushauri na tiba tunapatikana whatsapp/text no 0622925000
Usisahau kushare makala hii kwa ndugu marafiki na jamaa zako.
Masha Masanja
Thursday, 31 March 2016
JINSI YA KUTAMBUA KAMA UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILI WAKO
By: Masha Masanja
Call/txt/whatsapp 0622925000
Email: mashamasanja@gmail.com
Watu wengi tumekuwa tukiishi kwa kutojua miili yetu kama ipo sawa, hii ni kutokana na kile kitendo pengine cha kutougua hutufanya tujisahau kabisa katika kujua undani wa Afya yetu.
Leo napenda tujifunze namna ya kujua jinsi gani utatambua kuwa UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILI WAKO(BODY MASS INDEX kwa kifupi BMI)
Kwa kifupi kitendo hiki huhusisha vitu viwili ambavyo ni uzito wako katika kilogram(kg) pamoja na urefu wako katika mita(m). Tutajifunza kwa kutumia mfano.
Uhusiano huo upo katika mpangilio kama ifuatavyo:
BMI ikiwa chini ya 18.50 hapa inakuwa mtu huyu uzito wake upo chini kuliko kawaida(UNDER WEIGHT)
BMI kuanzia 18.50 hadi 24.99 huyu mtu ni mwenye Afya njema na yuko vizuri kabisa(HEALTHY)
BMI kuanzia 25.00 hadi 29.99 huyu ni mtu ambaye amezidi uzito(OVER WEIGHT) hivyo uzito wake na urefu wake haviendani kabisa.
BMI kuanzia 30.00 na kuendelea basi huyu mtu ni yule aliyepitiliza kabisa kiwango cha uzito na anaingia katika kundi la Obesity.
Sasa unapata vipi uhusiano wa uzito na urefu wako(BMI)?
Angalia hapa chini
Kanuni(BMI)=uzito ÷ (urefu)kipeo cha pili
Tuangalie mfano mimi Masha nina uzito wa kg 64 na urefu wa sentimeta 162 ambao ni sawa na mita 1.62
BMI ya Masha=64/1.62×1.62
BMI=64/2.6244
BMI=24.386
Kwa mfano huo basi Masha yupo kwenye kundi salama japo bado kidogo tu afikie 25 ambapo siyo pazuri.
Sasa tufanye ya kwamba Masha ana uzito wa kilo 74 na urefu uleule
BMI= 74/2.6244
BMI=28.196
Hapa anakuwa OVER WEIGHT
Na endapo Masha ana uzito wa kg 91;
BMI=91/2.6244
BMI=34.6745
Hapa ni OBESITY!!
Ndugu msomaji wa makala hii nadhani sasa umeshafahamu namna ya kujua kama una uzito unaoendana na urefu wako, hivyo unaweza kujifanyia tathimini wewe mwenyewe.
NOTE: UREFU WAKO UWE KATIKA KIPIMO CHA MITA(METRE).
Unaweza ku-share zaidi makala hii kwa watu wengi kadri uwezavyo ili nao waweze kujifunza kama ulivyojifunza wewe.
Pia huwa ninatoa ushauri na mafunzo maalumu jinsi ya kupunguza uzito/kitambi na nyamazembe kwa kutumia chakula tu, chakula hicho kitaubadili mwili uwe mashine ya kuunguza mafuta.
Wednesday, 30 March 2016
Hebu angalia faida 50 za kufanya mazoezi ya viungo ndani ya mwili wako
Umuhimu wa mazoezi kwa afya bora na maisha marefu bila maumivu.
Moja ya mahitaji matano (5) mhimu ili kuishi baada ya oksijeni, maji, chumvi, na potasiamu; ni Mazoezi. Mazoezi ni muhimu kwa ajili ya afya zaidi ya kuwa na maumbile ya kuvutia (sex body), burudani au kitu kingine chochote.
Watu wengi hufuatilia kuhusu chakula tu, hata kama utakula vizuri vipi bila mazoezi mlo haujakamilika, kwa hiyo mazoezi ni mhimu kwa yeyote kama ilivyo kwa maji au chakula.
Hizi ndizo faida 50 za mazoezi
Zifuatazo ni moja ya sababu 50 mhimu za kufanya mazoezi kwa afya bora na maisha marefu bila maumivu:
1. Hukufanya ujisikie vizuri
2. Huongeza uwezo wa kujifunza
3. Hujenga uwezo wa kujistahi
4. Huongeza nguvu ya ubongo kufanya kazi
5. Huuweka mwili wako kuwa unaofaa (fit) na wenye uwezo
6. Huongeza afya ya akili yako
7. Huongeza kinga ya mwili
8. Hupunguza mfadhaiko/stress
9. Hukufanya ujisikie vizuri/mwenye furaha
10. Hukufanya usizeeke mapema
11. Huweka ngozi yenye mng’aro na yenye afya
12. Husaidia kupata usingizi mtulivu
13. Husaidia kuzuia ugonjwa wa kiharusi/strokes
14. Huongeza ufanisi katika makutano/joints za mwili
15. Huongeza nguvu za mishipa
16. Huondoa wasiwasi
17. Huongeza kumbukumbu
18. Husaidia kudhibiti ulevi/uteja
19. Huongeza uzalishaji
20. Huongeza uwezo wa ubunifu
21. Hupendezesha muonekano wa mwili
22. Huongeza uwezo wa kujiamini
23. Husaidia kuongeza nguvu juu ya malengo yako maishani
24. Huondoa tatizo la kukinaishwa na chakula
25. Huongeza miaka ya kuishi
26. Hukomaza mifupa
27. Huongeza afya ya moyo
28. Huongeza hali ya kuwa na msimamo
29. Huondoa homa ndogo ndogo mwilini
30. Huongeza hamu ya kula
31. Hudhibiti usawa wa lehemu/kolesteroli
32. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na baadhi ya kansa
33. Hushusha shinikizo la juu la damu/BP
34. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na kisukari
35. Huzuia kupatwa na ukichaa/uwendawazimu
36. Hupunguza au huzuia maumivu ya mgongo
37. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa mifupa
38. Hupunguza hisia/fikra za kujisikia vibaya au kupiga punyeto kwa vijana
39. Huzuia kupotea kwa mishipa
40. Huongeza nguvu na ustahimilivu
41. Huongeza ufanisi katika michezo
42. Huongeza uwezo wa kuvumilia maumivu
43. Huongeza usawa na ushirikiano wa mwili
44. Huongeza usambazaji wa oksijeni katika seli za mwili
45. Huongeza hali ya ufuatiliaji/concentration
46. Huongeza uwezo wa kujitawala na kujidhibiti nafsi
47. Huondoa uchovu
48. Huongeza nguvu katika tendo la ndoa
49. Hufanya maisha kuwa yenye kuvutia zaidi
50. Huongeza ubora wa maisha
Mazoezi yafuatayo ni mazuri sababu ya thamani yake ya baadaye na hayasababishi maumivu kwenye maungio, nayo ni; kutembea kwa miguu, kuogelea, kuendesha baiskeli, kucheza tenisi, gofu, kukwea, kuruka kamba, kudansi na kadhalika.
Tafadhari share makala hii ili na wengine wajifunze kama wewe
Naitwa Masha Masanja, mshauri wa Afya. Pia ninatoa program maalumu kwa mtu anayehitaji kupungua uzito/kitambi au nyamazembe.
Mawasiliano:
0622925000 - whatsapp
0767925000
0784925000
Wednesday, 16 March 2016
ZIJUE NJIA ZA KUPATA PESA
Robert Kiyosaki ambaye ni mwandishi wa Kitabu kiitwacho “ Rich Dad Poor Dad” ameainisha njia nne za kupata fedha na kuwekeza.
Nimeona ni vema kuwashirikisha wasomaji wangu njia hizo na kuzidi kuwapatia dondoo zaidi za uwekezaji. Kwa jinsi ambavyo Robert Kiyosaki ameandika fedha zinapatikana kwa njia zifuatazo:
1. Kuajiriwa (employment)- ukiajiriwa unalipwa mshahara na malupulupu mbalimbali lakini unafanya kazi ya mtu mwingine.
Ingawa siyo lazima kufanya kazi wakati wote lakini Kiyosaki alisema “fanya kazi ujifunze au kwa kiingereza work to learn”.
2. Kujiajiri (self-employment)- hapa unajiajiri kama mjasiriamali lakini pia biashara yako inakuwa ndogo na unakuwa umeajiriwa lakini kwenye biashara yako.
Faida yake ni kwamba unakuwa huru na unakuwa wa kukua. Lakini usipopambana ukue unaweza kupata kipato kidogo kuliko hata watu walioajiriwa.
3. Biashara (business) –hapa unamiliki biashara ambayo umeajiri watu wengine wanaofanya kazi kwa ajili yako. Kazi yako inakuwa ni usimamizi na kuhahakikisha biashara inakua.
Ukifika hapa uwezekano wa kukua ni mkubwa kama utakuwa kiongozi mwenye mikakati.
4. Kuwekeza (investment) –hapa unawekeza kwenye rasilimali “assets” ambazo zinakupa kipato hata kama haupo (passive income).
Kwa hapa unaweza kuwekeza kwenye nyumba, ardhi, taasisi za fedha (financial institution) kama kwenye account za muda maalum, hati fungate, hisa n.k.
Usikubali hela yako hata shilingi laki moja ikae bure hata kwa mwezi zipo njia za kuwekeza.
Saturday, 12 March 2016
Angalia mtazamo kuhusu Elimu na Ajira, bado Ujasiriamali unahitajika tu

Tatizo la ajira litakoma tu kama mitazamo yetu itabadilika kuanzia ngazi ya familia mpaka ngazi ya kitaifa mtazamo huu:
Familia zetu zinatakiwa kujua tu kuwa mtu haendi shule ili aje afanye tu kazi za kuajiriwa maofisini kwenye kiyoyozi lakini familia zilenge kumpeleka shule mtoto ili apate ujuzi utakao muwezesha kupambana na mazingira na soko la ajira ambalo linahitaji sana ujuzi na uwezo kuliko vyeti.
Familia pia ijenge utamaduni wa kuandaa mifuko ya miradi itakayo wawezesha watoto wao kujiajiri mara wamalizapo shule.
Familia zetu pia ziwe na utamaduni wa kufuatilia masomo ya kijasiriamali kupitia runinga na hata vinginevyo ziweze kuwafungua. Wazazi wajue namna ya kuwa control watoto wao kuangalia vitakavyowajenga katika mtazamo chanya tokea wako watoto.
Pili upande wa makanisa ni kuwa tusi hubiri sana muujiza wa maisha, maisha siyo muujiza ni uhalisia.
Waumini wafundishwe kinaga ubaga kwamba bila kufanya kazi maisha hayatabadilika hata kama mtu ananena kwa lugha.
Familia itengeneze mfumo unaowezekana wa kuwatambua watu wasio na kazi na kanisa liwawezeshe.
Makanisa yaandae semina na vipindi mbalimbali vya kufundisha masomo ya ujasiriamali na Elimu ya kuweka akiba. Makanisa yamekuwa yakihubiri sana Neno la MUNGU na wamesahau kuwa Neno bila fedha haliwezi kuhubiriwa.
Tatu upande wa serikali ni kwamba serikali inahitaji kuingiza somo la ujasiriamali kuanzia shule ya msingi mpaka vyuo vikuu ili kuwajenga wanafunzi waweze kujua umuhimu wa kujiajiri.
Serikali pia inatakiwa kupunguza miaka ya kustaafu kwa watumishi wa umma kwa mtazamo kwamba watumishi wa umma wafanye kazi kwa mkataba say wa miaka 10-15 na walipwe mishahara inayoonekana na wasisitizwe kuwekeza maana baada ya miaka hiyo wataondoka ili kupisha mawazo na watu wengine kuingia kazini.
Haiwezekani unampa mtu astaafu baada ya kufikisha miaka 60. HAPA ndo watu wanajisahau wanakufa maskini Pamoja na kuwa walikuwa wanapokea mishahara mikubwa.
Serikali pia ifanye mpango wa kuwatambua wanafunzi wenye uwezo mkubwa wa kuanzisha makampuni na iwawezeshe ili wanafunzi hao waajiri wanafunzi wengine. Serikali itoe fursa kwa wanafunzi wa mwaka wa mwisho kuandika mawazo ya kibiashara na yale yanayowezekana yawezeshwe na watu waanze mara moja wamalizapo.
Mwisho upande wa mtu binafsi.
Kimsingi tatizo hili linaanza na sisi wenyewe.
Jim Rhon anasema "kama utabadilika kila kitu kitabadilika".
Kuna haja sasa mtu binafsi kuanza kubadili mtazamo wake hasa kwa wasomi.
Amini kuwa siyo lazima uajiriwe na mtu ofisini na kumbe unaweza fanya mambo yako na ukifika mbali.
Anza na kile ulichonacho (capital accumulation) na baade utafika mbali usisubiri mitaji mikubwa.
Penda maarifa kwa kusoma vitu vizur vitakavyo kusaidia.
Maisha ni vile utakavyoamua wewe yawe. Hakuna mtu mwenye uweze wa kutengeneza maisha yako. Wewe ndo pekee wa kuweza kubadilisha maisha kwa kuwa ndo dereva wa maisha yako.
Namaliza kwa kusema Inawezekana "what was impossible yesterday is possible today".
Wajibika..!!
Masha Masanja
0622925000
Friday, 11 March 2016
YAONE MAAJABU YA SABUNI HII ILIYOTENGENEZWA KWA MAGAMBA YA VIUMBE WA BAHARINI

Ni sabuni iliyotengenezwa kutokana na magamba ya viumbe wa baharini kama simbi, konokono na viumbe wengine wa baharini.
Magamba hayo yanasagwa na kutolewa ili kutengeneza sabuni hii bora.
Sabuni hii ina aina18 za amino acid..zaid ya aina 30 za Trace Element na vitamins ambazo zinasafirisha material yenye virutubisho ndani ya ngozi na kuondoa vitu vigeni katika ngozi yako
KAZI ZAKE
1. Kutengeneza uzuri wa ngozi iwe na ubora wake.
2. Inaimarisha uasili wa ngozi.
3. Inaondoa mafuta na jasho na kuifanya ngozi kubaki kavu na safi.
4. Inasafisha na inaondoa sumu ndani ya ngozi.
5. Inaondoa mabaka na upele.
6. Kuponya muendelezo wa tishu zilizoharibika ndani ya ngozi.
7. Kuondoa mafuta yaliyoganda na kuziba vinyweleo na kuifanya ipumue vizuri
8. Inaondoa chunusi na kuifanya sura ing'ae.
9. Inang'arisha ngozi
10. Inazuia uharibifu wa ngozi unaotokana na miale ya jua na miali yenye kemikali nyingine kupitia ngozi.
11. Inaondoa mba wa shingoni, mwilini na hata kichwani.
12. Inaondoa Fangasi za aina zote hata kwa wanaonuka miguu wameliwa vidole wakivua viatu.
Utaalamu huu wa kutumia viumbe wa bahari katika usafi na uimara wa ngozi ulianza karne nyingi nchini china na unaendelea hadi leo na hata wazee wa Kichina hawachoki ngozi na akili.
Ni nzuri kwa wanawake, wanaume watoto, vijana na wazee...!!
MATUMIZI
1. Loweka ngozi kwa maji safi.
2. Paka sabuni juu ya ngozi.
3. Sugua kwa dakika 1 - 3.
4. Suuza kwa maji safi.
5. Tumia mara 2 kwa siku kupata matokeo mazuri
Enjoy harufu nzuri na isiyoumiza pua zako yenye kukufanya upende kuendelea kuoga tu muda wote...! Harufu salama ya maua na zabibu..!
ANGALIZO
Sabuni hii haijatengenezwa kwa kemikali za viwandani ni Tiba mbadala, hivyo unashauriwa kuitumia na kutokupaka vipodozi vya kemikali, hasa Lotion zenye hydroquinone, ina maana utakuwa unatibu Kisha unajeruhi tena, Tumia Lotion zisizo na kemikali.
Kwa kuzipata sabuni hizi wasiliana nami hakika hutaogea sabuni nyingine yenye kemikali tena maana ni sabuni salama kabisa.
Whatsapp 0622925000
Call 0767925000
Monday, 7 March 2016
MAMBO MUHIMU YA KUFANYA UNAPOTAKA KUANZA BIASHARA YA MTANDAO

Watu wengi wamekuwa wakibabaika wanapokabiliwa na watu Kuchagua kampuni ya mtandao wanaowafuata na kuwashawishi kujiunga na kampuni za mitandao au pale wanapokuwa wameamua kwa mapenzi yao kuingia kwenye biashara za mtandao wasijue namna ya kutoa maamuzi sahihi kwamba ni kampuni ipi au zipi ndizo bora kujiunga nazo.
Kwa maoni yangu, hii ndiyo hatua muhimu kuliko zote kwa sababu endapo utaangukia kwenye mikono ya kampuni mbovu, nguvu zako na mtaji wako vyote ni bure. Leo katika ukurasa huu tutaona vigezo vya kuvitumia katika kuchagua kampuni ya mtandao ya kujiunga nayo. Moja kwa moja nitaanza kwa kuviorodhesha vigezo hivyo au sifa za kampuni bora na kuvitolea maelezo.
1. Historia Ya Kampuni
Zipo kampuni ambazo zinaanza biashara na baada ya muda mfupi zinapotea au kufilisika. Kama ulikuwa mmoja wa wanachama wa kampuni ya namna hiyo, lazima utakuwa umeathirika kwa namna fulani. Inabidi upate kampuni ambayo ina historia ya kufanya biashara kwa muda mrefu, kwa ufanisi na ambayo biashara yake bado inaendelea kukua na si ile ambayo imefikia ukomo. Njia rahisi ya kupata taarifa hii ni kupitia internet ingawa kuwauliza ndugu na marafiki wengine inaweza kusaidia pia.
2. Bidhaa Za Kampuni
Kampuni bora ya mtandao ni ile ambayo bidhaa zake zinalenga kutatua matatizo ya wateja katika jamii unayoishi na zimethibika kufaulu katika kufanya hivyo. Bidhaa ambazo zitatangazwa halafu zikashindwa kukidhi mahitaji ya wateja zitakuwa na muda mfupi sana wa mauzo kabla ya wateja kugundua kuwa haziwafai. Bidhaa zitakazokidhi haja ya wateja zitakurahisishia kazi wewe muuzaji kwani baadaye zitajiuza zenyewe. Bidhaa hizo pamoja na kutatua matatizo ya wateja ziwe na bei ambazo wateja wengi wataweza kuzimudu kwani pamoja na ubora wake bidhaa ambayo bei yake itakuwa juu mno itauzika kwa wateja wachache sana wenye uwezo. Kumbuka kuwa wewe kama mwuzaji utanufaika zaidi pale unapouza bidhaa kwa wingi zaidi.
3. Mpango Mzuri Wa Ulipaji (Compensation Plan)
Mpango mzuri wa ulipaji na ambao ni rahisi kuuelewa ndio utakaokupa wewe pesa. Kama kampuni haina mpango mzuri wa ulipaji kamwe hutapata pesa ya kutosha na kama mpango wao si rahisi kueleweka utakosa pesa nyingi kwa sababu ya kutojua namna ya kuitumia kampuni yako vizuri.
Kwa vile ulijiunga na kampuni ya mtandao ili upate pesa ya kuboresha maisha yako, kitu cha kwanza cha kutazama ni mpango wao wa ulipaji na kuusoma au kuupitia kwa makini. Hili ndilo kosa ambalo watu wengi hulifanya, kujiunga na kampuni na kuanza kuchakarika bila kuujua kwa undani mpango wa ulipaji wa kampuni yake.
Monday, 29 February 2016
HOSPITALI YA WILAYA YA KISHAPU YAWA MSAADA KWA WAKAZI WA WILAYA YA KISHAPU NA MAENEO YA JIRANI
![]() |
| Add caption |

Kuanza kufanya kazi kwa Hospitali ya Wilaya ya Kishapu kumeelezwa kuwa ni msaada mkubwa kwa wadau wa huduma ya Afya hususani wagonjwa kutoka ndani ya Wilaya ya Kishapu
Hayo yamethibitishwa na baadhi ya wagonjwa wanaoenda kupata huduma katika Hospitali hiyo ambayo ipo jirani kabisa na eneo la Halmashauri ya Wilaya.
Hospitali hiyo ambayo ni ya Serikali imekuwa msaada mkubwa na wagonjwa wamekuwa wakimiminika kwa wingi kutokana na baadhi ya makundi ya wagonjwa kupatiwa huduma bila malipo kutokana na sera ya Serikali katika kutoa Huduma ya Afya. Makundi hayo ni pamoja na wazee kuanzia umri wa miaka 60, akinamama wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano.
Mmoja wa wagonjwa aliyehojiwa na mwandishi wa makala hii alidai yeye anatokea kijiji ya Mwakipoya alidai yeye amekuja Hospitalini hapo kwa kuwa amesikia habari kutoka kwa baadhi ya watu waliowahi kutibiwa hapo kuwa wagonjwa wamekuwa wakipata huduma zote hususani Vipimo na Madawa.
Wagonjwa kutoka vijiji vya Wilaya za jirani za Maswa na Meatu pia wamekuwa wakifika Hospitalini hapo kujipatia huduma.
Mbali na makundi hayo yanayopata huduma bila malipo lakini pia makundi mengine yamekuwa yakijipatia huduma kwa gharama za kawaida ikiwemo familia zinazochangia mchango wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii(CHF) pamoja na wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF)
Wakielezea mapungufu wanayoyaona mara wanapoenda kutibiwa Hospitalini hapo, baadhi ya wagonjwa wamedai Hospitali bado inaonekana kuwa na Watumishi wachache kwani muda mwingine wamekuwa wakishuhudia Muuguzi mmoja au wawili wakilazimika kuhudumia Wodi zote za Wanaume, Wanawake, Wazazi na hata sehemu ya Huduma ya Wagonjwa wa nje(OPD). Hivyo wagonjwa wameomba jambo hilo lifanyiwe kazi na mamlaka husika kwani wao(wagonjwa) wamefurahi kufunguliwa kwa Hospitali hiyo maana imekuwa ni msaada kwao na imewaepusha gharama za usafiri kwa wakaazi waliokuwa wakienda kupata Huduma katika Kituo cha Afya Kishapu kilichokuwa kikitumika zamani kwa wakaazi wote. Kituo hicho cha Afya kilichokuwa kikitumika zamani kipo umbali wa zaidi ya Kilometa 8 kutoka mji wa Mhunze.
Hospitali ya Wilaya ya Kishapu ilianza kufanya kazi katikati ya mwezi Novemba 2015 na ina majengo na vifaa vyote vya Huduma ya Wagonjwa wa Nje(OPD), Huduma za kulaza Wagonjwa(IPD), Wodi ya Wazazi(Maternity Ward), Jengo la Upasuaji na Mochwari.
Jina linalotumika kwa Hospitali ni Dr. Jakaya Mrisho Kikwete District Hospital
Sunday, 28 February 2016
TABIA MBAYA 10 ZINAZOFANYA USHINDWE KUWA NA AKIBA "SAVINGS"....HATIMAYE UNAKOSA MTAJI WA KUFANYA MAMBO YAKO..

1.Unanunua nguo bila mpangilio..
Kuna watu wana nguo kama duka. Plz Kuwa na nguo chache Tu huwezi kushindana na fashion.
2.Unanunua Viatu bila mpango.
Viatu pia vinameza savings zetu. Nunua pea chache zenye ubora ili zidumu.
3.Unatoa ofa bar bila mpango.
Nenda bar kwa bajeti mahususi. Hakuna atakae kusifia kwa kutoa ofa hovyo. Kila mbuzi ale kwa urefu Wa kamba yake. Jifunze ubepari.
4.Unatumia hela nyingi kwenye simu ambazo sio productive. Unaweka vifurushi vya week vya sh 7000 au 10000 ili uchati na marafiki Fb au wasaap Huo ni ujinga. Badilika.tumia internet kujifunza tumia internet kwa mambo ya kukupa biashara yako.
5.Unakopa hela benki na kununua vitu kama simu ya milioni na gari ambazo sio productive. Unakosa hela hata ya mafuta, gari la nini kwanini usingewekeza sehemu ili kuwe na mradi Wa kuzalisha ndio ununue gari?
6.Una marafiki wengi ambao ni mizigo kwako au hamuendani kivipato hivyo unajikuta unalazimika kutumia zaidi ya kipato chako ili uwa-impress. Meneja Wa TRA na mwalimu Wa sec unatarajia utoe offer mpaka umfurahishe meneja? Utabaki na sh ngapi toka kwenye salary yako?? Zinduka.
7.Huna timetable ya kudumu ya maisha yako, unajikuta unaburuzwa Tu na marafiki zako kwa kwenda sehemu mbalimbali za matumizi.
Kuwa na ratiba za maisha yako na zisimamie kikamilifu, usiburuzwe!
8.Una michepuko inayokutegemea wewe kwa kila kitu. Wanakuita ATM we we unakenua Tu huzinduki. Badilika.
9.Una huruma sana kuliko kipato chako. Yaani kila ukiombwa unatoa hata kama muombaji hana genuine need. Usiwe mkristo kuliko Yesu. Fanya hivyo kama ni lazima. Ila sio kila anaekupiga mzinga unapigika.
10.Unatembea na hela nyingi kwenye wallet au mshahara wote kwenye wallet au handbag au nyumbani kwako. Unapokuwa na petty cash nyingi unatengeneza mazingira ya kutumia hovyo. Jifunze kuweka hela benki. Tembea na hela Tu unayoihitaji kwa matumizi ya lazima.
Naamini tukizingatia kanuni hizi kumi tutaongeza savings zetu na kuwa na mtaji Wa kufanya vitu vikubwa endelevu.
Saturday, 27 February 2016
Zijue fursa 150 za biashara Ulimwenguni
Zijue Fursa 150 za biashara na miradi mbalimbali nchini Tanzania
1. Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha.
2. Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha.
3. Kutengeneza na kuuza tofali
4. Ufundi, Website updating/Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na Makampuni mbalimbali.
5. Kuanzisha kituo cha redio na televisheni
6. Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na vifaa vya compyuta na mawasiliano.
7. Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k
8. Kushona na kuuza nguo.
9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali,
10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Kuku, Bata, na wengine.
11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo.
12. Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu.
13. Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza popcorn na kuziuza.
14. Kusajili namba za simu na kuuza vocha
15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta na zinazotumia mafuta
16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika.
17. Kuuza Mitumba
18. Kusimamia miradi mbalimbali
19. Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali
20. Kufungua banda la chakula na chips
21. Kukodisha turubai viti na meza
22. Kufungua Supermarket
23. Kufungua Saluni
24. Kufungua Bucha
25. Video Shooting & Editing.
26. Kufungua Internet cafe
27. Duka la kuuza matunda
28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline.
29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement, vifaa vya umeme, duka la mabati
30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi ya ICT
31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k
32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor)
33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k
34. Kuuza maji kwa jumla na rejaleja.
35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora.
36. Kukodisha Music
37. Kuanzisha Mradi wa Taxi
38. Kuanzisha mradi wa Daladala
39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters, HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa vingine.
40. Kununua magenerator na kukodisha
41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu
42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP)
43. Kuuza mabati na vigae
44. Kujenga apartments
45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote
46. Kufungua Duka la samaki
47. Kufungua Duka la nafaka
48. Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo.
49. Kujenga hostel
50. Kuuza vocha na ving’amuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental.
51. Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda na wananchi.
52. Ufundi simu
53. Kufungua Hospitali, Zahanati.
54. Maabara ya Macho, Meno
55. Kuchimba/Kuuza Madini
56. Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na fax
57. Kuuza miti na mbao
58. Kufungua Grocery, bar
59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha
60. Kucharge simu/battery
61. Duka la TV na vifaa vingine
62. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na tamasha mbalimbali (catering).
63. Banda la kupigisha simu
64. Kuuza na kushona Uniform za shule
65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla.
66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari
67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe
68. Kuuza fanicha
69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi
ya magari na mitambo.
70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel)
71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium.
72. Kuuza vioo
73. Kushona na kukodisha nguo za harusi
74. Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari
75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine).
76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc)
77. Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi
78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya redio na televisheni
79. Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games)
80. Kufungua benki
81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga
82. Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k
83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali
84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane)
85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu.
86. Kuanzisha viwanda mbalimbali
87. Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali zinazoendana na mawasiliano ya Vodacom, TTCL, AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k.
88. Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe, mikutano mbalimbali
89. Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa barabara na kukodisha
90. Kutengeneza antenna na kuuza
91. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao
92. Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo
93. Biashara ya kuagiza magari
94. Kufanya biashara za Jukebox
95. Kukodisha matenki ya maji
96. Kufungua duka la kuuza Asali
97. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha
98. Kufungua Duka la vinyago, batiki
99. Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZY PESA
100. Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym).
101. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi.
102. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy).
103. Kufungua Kampuni ya Ulinzi
104. Kufungua kampuni ya "Clearing and fowarding"
105. Kuchezesha vikaragosi
106. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki
107. Kuuza baiskeli
108. Kuuza magodoro
109. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe, vijiko,
110. Kuuza marumaru (limestones)
111. Kuuza kokoto
112. Kuuza mchanga
113. Kufundisha Tuisheni
114. Biashara za bima
115. Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya anga (ndege)
116. Biashara za kitalii
117. Biashara za meli na maboti.
118. Kampuni ya kuchimba visima
119. Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa kujitegemea
120. Kuuza mkaa
121. Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali
122. Kampuni ya kupima ardhi
123. Kampuni ya magazeti
124. Kuchapa (printing) magazeti
125. Kuuza magazeti
126. Kuchimba mafuta
127. Kiwanda cha kutengeneza mabati
128. Kiwanda cha kutengeneza fanicha
129. Kiwanda cha kutengeneza matairi
130. Kutengeneza vitanda vya chuma
131. Kununua nyumba katika Maghorofa (Apartments) na kuzikodisha.
132. Kukodisha makapeti
133. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe.
134. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka.
135. Kazi ya ususi na kusafisha kucha.
136. Kuuza Gypsum
137. Malori ya kubeba mafuta na Mizigo
138. Duka la kuuza mboga za majani
139. Duka la kuuza maua.
140. Kampuni ya kuzoa takataka
141. Kampuni ya kuuza magari
142. Kuuza viwanja
143. Uvuvi
144. Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea fensi
145. Uchoraji wa mabango.
146. Duka la kuuza silaha
147. Ukumbi wa kuonesha mpira
148. Biashara ya mlm (network marketing)
149. Yadi kwa ajili ya kupaki magari
150. Mradi wa trekta za kukodisha kwa ajili ya kilimo
Friday, 26 February 2016
SABABU ZINAZOPELEKEA BIASHARA YAKO KUFA HATA KAMA NI YA MTAJI MKUBWA AU MDOGO

Mara nyingi wengi wanaoingia kwenye biashara kwa mara kwanza huamini sana mtaji ndio kila kitu. Kwa imani hiyo, hujikuta mara baada ya kuingia kwenye biashara wanakuwa hawaweki nguvu nyingi katika maeneo mengine muhimu ili kuboresha biashara zao. Na matokeo yake hupelekea biashara hizo kuanza kufa huku zikiwa zina mtaji mkubwa kabisa.
Kinaweza kuonekana ni kitu cha kushangaza lakini huo ndio ukweli. Unajua ni kwa nini ? Ni kwa sababu waliaminishwa toka siku nyingi kwamba ukiwa na mtaji mkubwa basi, kila kitu kimekwisha. Lakini, leo katika makala yetu tutaangalia sababu zinazoweza kupelekea biashara yako ikafa, hata kama ina mtaji mkubwa.
Kwa kupitia makala haya itakuonyesha na kukupa ukweli wa wazi kwamba, mtaji mkubwa peke yake sio ‘gerentii’ ya kukufanya wewe ukafanikiwa kibiashara. Yapo mambo mengine ya ziada ambayo unatakiwa kuyazingatia na kuyatilia mkazo kila siku, ili biashara yako iweze kukupa yale matunda unayoyataka.
Kumbuka haijalishi biashara yako ina mtaji kiasi gani, lakini elewa ukweli huu inaweza ikafa usipozingatia mambo haya ya msingi. Sasa nataka twende pamoja kujifunza na kujua mambo au sababu zinazoweza kupelekea biashara yako ikafa, hata kama ina mtaji mkubwa vipi. Karibu sana tujifunze pamoja.
1. Kukosa usimamizi imara.
Kama unaona unataka kuanzisha biashara yako, halafu ukagundua huna usimamizi imara ni bora ukaachana na hiyo biashara. Na kama ungekuja kwangu leo na kunieleza hali hiyo ilivyo, ningekushauri hivi ‘ Chukua pesa hizo kisha nenda mjini, katafute sehemu wanakochoma nyama nzuri kula pesa yote usibakize hata Shilingi mia moja.’
Sikutanii. Kwa nini nakwambia hivyo, kufanya biashara yako huku ukiwa huna usimamizi wa kutosha ni sawa na kupoteza pesa hizo. Tena unazipoteza bila kufaidi hata tone. Hapa unaona hata kama ungekuwa na mtaji mkubwa vipi, kama huna usimamizi ni lazima biashara hiyo itakufa tu, hakuna ubishi.
2. Kukosa elimu ya biashara.
Najua umeshawahi kusikia sana fulani alipata mkopo wa benki milioni sitini, lakini biashara zake zimekufa. Unajua chanzo chake kimojawapo ni nini? Ni kukosa elimu ya biashara. Wengi wanapokosa elimu hii huwekeza kiholela sana matokeo yake kupoteza pesa nyingi bila sababu ikiwa pamoja na mtaji.
Kwa hiyo ili kufanikiwa kibiashara ni lazima wewe kuwa na elimu ya kutosha kibiashara. Pengine unataka kujiuliza nitaipata wapi sasa? Sikiliza huhitaji gharama kubwa sana kuipata. Unaweza kujifunza kupitia semina, huwezi hilo unaweza kujifunza kupitia mitandao ya kuhamasisha au ukanunua vitabu vinavyohusu biashara ukajifunza polepole. Lakini kikubwa usiikose elimu hii, vinginevyo utapoteza mengi ikiwa pamoja na biashara yako.
3. Matumizi mabaya pesa.
Sio kwa sababu biashara yako ina mtaji mkubwa na inaingiza pesa nyingi kwa siku, basi na matumizi yako yanakuwa yako juu bila sababu. Kama unafanya hivyo kwenye biashara yako nikupe tu uhakika huu, huwezi kufika mbali. Ni lazima uwe na mpangilio mzuri wa matumizi yako ya pesa ili kuifanya biashara yako ikazidi kuendelea.
Acha kujidanganya kwa kuendelea kutumia pesa vibaya, utazipoteza zote mpaka utashanga. Kikubwa unajua jinsi huo mtaji ulivyoupata. Kama ni hivyo kwa nini uutumie hovyo? Kuwa makini na pesa zako. Tofauti na hapo biashara yako itakufa tu hata kama sio leo, lakini lazima itakufa.
4. Kukosa ubunifu.
Ili uweze kukabiliana na ushindani, ubunifu ni muhimu sana katika biashara yako. Bila kuwa mbunifu huwezi kufanikiwa katika hiyo biashara kutokana na mazingira ya ushindani mkubwa tulionao kwa sasa. Kwa hiyo ni lazima kuwa mbunifu na kuifanya biashara yako ikaonekana ya tofauti na kukupa wateja wa kutosha.
Wengi wanaoshindwa kwenye biashara ni wale walioingia kwa kiburi cha mtaji mkubwa na kusahau ubunifu. Haijalishi unafanya biashara ndogo au kubwa weka ubunifu. Kila wakati tafuta ni kitu gani biashara yako inakosa, kisha kiboreshe zaidi. Jitahidi sana kuweka ubunifu ili kuifanya biashara yako iwe hai siku zote, vinginevyo utaiua.
5. Kukosa nidhamu.
Kama unaendesha biashara yako na ukakosa nidhamu ya kuiendesha biashara hiyo, elewa kabisa utakuwa na mchango mkubwa sana wa kuiua. Nidhamu ni msingi mkubwa sana wa mafanikio yoyote na sio biashara tu peke yake. Jaribu kuangalia watu wote wenye nidhamu ya kazi mafanikio yao yakoje? Bila shaka ni makubwa.
Biashara nyingi sana zinazokufa huku zikiwa na mtaji mkubwa mara nyingi hukosa nidhamu. Tuchukulie una duka la reja reja, huwezi kufanikiwa ikiwa unafungua na kufunga unavyotaka. Ni lazima uwe una nidhamu ya muda, nidhamu ya kuwajali wateja au nidhamu ya kauli nzuri. Kwa kukosa nidhamu hizi biashara itakufa tu hata iwe kubwa vipi.
6. Kukosa wateja.
Kati ya kiungo muhimu sana kwenye biashara yako ni wateja. Bila wateja hakuna biashara inayoweza kufanyika. Sasa kama utakuwa huna wateja hiyo inamaanisha biashara yako kwa vyovyote vile itaenda kufa hata ufanye nini. Maana hao ndio wawezeshaji wakubwa kwenye biashara yako kuendelea.
Sasa huwa zipo sababu zinazopelekea biashara hii ikakosa wateja na nyingine ikawa na watej wengi. Hivyo ni vyema ukazijua sababu hizo ili zikusaidie kuweza kujenga biashara ya uhakika na yenye mafanikio makubwa.
7. Kukosa vipaumbele.
Biashara yoyote iwe inanza au inaendelea ni lazima iwe na vipaumbele vya msingi ambavyo vinatakiwa vifuatwe kila siku. Kama kipaumbele chako kimojawapo ni kutaka kukuza mtaji ni vyema ukawa makini kuhakikisha hilo linatimia na kutekelezeka kwa haraka sana.
Lakini kama pia vipaumbele vyako ni kuhakikisha unadumisha mahusianao mazuri na wateja wako, pia ni bora ukatekeleza. Unapokosa vipaumbele hata vile unavyoviona ni vidogo ni rahisi sana kwa biashara yako kuweza kufa na kushindwa kuendelea hata kama ina mtaji wa kutosha. Kwa sababu hapa tunasema biashara inakuwa inakosa dira maalumu.
8. Kukosa mgawanyo wa majukumu.
Pia biashara inaweza ikafa hata kama ina mtaji wake mkubwa, ikiwa itakosa mgawanyo wa majukumu. Ni lazima biashara iwe na mgawanyo wa majukumu ili iweze kusonga mbele. Kama unaona unafanya biashara huku kila kitu umeshikilia wewe na hakuna wa kukusidia elewa upo kwenye hali mbaya.
Ni lazima utafute watu wa kukusaidia hata kama pale haupo mambo yaweze kwenda sawa kabisa. Siri mojawapo kubwa ya kufikiwa mafanikio makubwa kwenye biashara yako ni kutengeneza mgawanyo mzuri wa majukumu kwa wasaidizi wako. Kushindwa kufanya hivyo ni lazima utaua biashara yako.
Hivyo kabla hujafanya chochote unapotaka kuanzisha biashara hakikisha hayo mambo utayahimili.
Kwa ushauri na mafunzo zaidi ya biashara wasiliana nami:
0767925000
0622925000 - whatsapp
Email: mashamasanja@gmail.com
Monday, 22 February 2016
BIASHARA UNAYOWEZA KUIFANYA MUDA WAKO WA ZIADA
Wengi hatujui inavyofanya kazi na maajabu yake.
Call: 0767925000
Whatsapp: 0622925000
Wednesday, 23 December 2015
MADHARA YA KUTUMIA VIDONGE VYA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA GHAFLA
Hivi ni vidonge vinavyotumiwa sana na miongoni ya wanaume au vijana wengi kwa lengo la kuongeza uwezo wao wa kufanya mapenzi. Dawa hizi hutumiwa zaidi na wanaume wasioweza kusimamisha uume vizuri(low libido) kwa leo la kumuwezesha kukidhi haja zake au za mwenza wake wa kike. Lakini pia zimekuwa zikitumiwa na vijana wengi kwa lengo la kumkomoa mwanamke au wengine hufanya kwa kuiga kutoka kwa waigizaji video za ngono(pornograph). Madhara ya vidonge hivi ni mengi, leo tutayajua
JINSI VINAVYOFANYA KAZI
Viagra haimfanyi mtu kupata hamu ya ngono bali yenyewe hufanya kazi endapo tu mtu atakuwa na hamu ya kufanya ngono. Hebu tugusie kidogo kuhusu uume unavyoweza kusimama.
Pindi mwanaume anapopata hamu ya kufanya ngono, mishipa ya fahamu iliyoko katika misuli ya uume hutoa chemicals zinazoitwa "nitric oxide" ambayo huamrisha viamshi(enzymes) kuzalisha chemicals nyingine tena zinazoitwa "messenger cyclic guanoside monophosphate". Hali hii huifanya misuli laini ya uume kujiachia na kutanuka ambapo matokeo yake huiruhusu damu kuingia na kujaa vizuri katika mishipa midogomidogo iliyoko katika uume(cappilaries), hapo ndipo uume unakuwa umesimama vizuri.
Hivyo basi, Viagra hufanya kazi ya kusawazisha kiwango cha hii kemikali inayoitwa Cyclic guanosine Monophosphate.
SASA TUONE MADHARA YA VIDONGE HIVYO
Kwa mara ya kwanza dawa hii ilitumika kutibu tatizo la Presha, lakini ilionyesha maajabu pale ilipooneka kuwafanya wagonjwa kuwa na nguvu nyingi za kusimamisha maumbile yao ya uzazi. Baada ya hapo zikazuiliwa kutumika mahospitalini lakini baadae zikafanyiwa uchunguzi na zikaanza rasmi kutumika kwa wanaume wenye matatizo ya kusimamisha. Kipindi hicho watu wenye matatizo ya kusimamisha walikuwa wakipewa dawa hii chini ya uangalizi wa Daktari huku wakipewa ushauri wa kutosha kwamba wataweza kusimamisha na hivyo Saikolojia hiyo ikawakaa na wakasimamisha, lakini baada ya muda fulani, mgonjwa wa tatizo hurudi katika hali yake ya kutosimamisha.
MADHARA
=>Mtu anayetumia vidonge hivi bila usha wa Daktari huku akiwa na matatizo mengine ya Kiafya kama Presha yuko hatarini kupoteza uhai wake.
=>Matumizi makubwa ya dawa hizi hufanya tatizo kuwa kubwa zaidi kwa sababu dawa hizi humfanya mtu kusimamisha kwa muda tu kwani akihitaji kufanya mapenzi siku nyingine inampasa ameze tena. Hali hii ya kuzimeza kila wake inamfanya kuwa dependant(tegemezi) na kumfanya azidi kuongeza dozi zingine na mwiso wa siku hutengeneza sumu mwilini na kuua kabisa nguvu za kiume.
=>Madhara mengine ni kupoteza uwezo wa kusikia(ukiziwi) pamoja na kupoteza uwezo wa kuona.
Kuliko kutumia vidonge hivyo, ni vyema ukatumia vidonge visivyo na madhara ambavyo havina kemikali yoyote. Mimea ya butea superba imeonyesha kiwango kiwango kikubwa cha kutibu kabisa tatizo la upungufu wa uwezo wa kusimamisha. Mmea huu unalimwa nchini Thailand na watafiti wa tiba asili wameamua kuutengeneza mmea huu katika mfumo wa vidonge ili iwe rahisi kupatikana katika nchi zote.
Hata hapa Tanzania vidonge hivi vilivyotengenezwa kwa mmea huu wa Butea Superba vinapatikana kirahisi tu hasa mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Morogoro, Tanga na Dar es salaam.
CONTACTS:
0784925000
0767925000
0622925000 whatsapp
Email: mmasanja86@gmail.com


Tuesday, 22 December 2015
WANAUME: CHAKULA NA NGUVU ZA KIUME

Kama tulivyowahi kueleza katika dondoo za afya huko nyuma jinsi ya kuboresha mwenendo wa maisha kiafya ni pamoja na ufanyaji wa tendo la ndoa kwa namna tuliyoieleza.
Na kabla ya kuvitaja hivyo vyakula kwa ufupi tuangalie sababu ya tatizo la kukosa hamu ya tendo la ndoa au upungufu wa nguvu za kiume.
SABABU
1.Vyakula hasa vyenye mafuta ya wanyama au mafuta yenye Lehemu(Cholestrols).
Matumizi ya vyakula vye kusindikwa zaidi.
2.Madawa, dawa kama Cimetidine ya vidonda vya tumbo au Adolmet ya shinikizo la damu la kupanda.
3.Miozi kama ya X-ray, Gamma Ray, simu,na vifaa vingine vya Electronic .
4.Magonjwa kama Sonona, Msongo wa mawazo, Kisukari, Kifafa, Ngiri n.k
5.Unene kupita kiasi(Obesity).
6.Kupendelea kuangalia picha za ngono au utupu.
7.Sigara.
8.Pombe.
9.Na nyinginezo.
Hizo ni baadhi ya sababu kwa ujumla wake.
Vyakula vyenye madini ya zinc, folic acid,Omega 3(Mafuta ya samaki), Vitamini B1, B6,B12, E n.k ni katika vyakula vyenye kuongeza hamu ya tendo la ndoa. Pia kuongeza ufanisi wa ufanyaji wa tendo la ndoa(Nguvu).
Baadhi ya vyakula hivyo ni vifuatavyo:
Tangawizi, Kitunguu swaum, Tikiti maji(hasa mbegu zake), Parachichi,Kitunguu maji, Asali, Habat sawda, Tende,Pilipili, Mdalasini, Karanga, Korosho,Pweza, Kiini cha yai, Mkate wa brown,Dark Chocolate, Mbegu za boga, Soya,Karoti, Ndizi mbivu n.k.
Vyakula hivi unaweza kula katika namna ya kuimarisha na kuboresha afya yako,lakini unaweza ukala katika namna ya kuimarisha hamu ya tendo la ndoa(Libido). Kwa leo tutaelezea juisi ya tende na tikiti maji.
Kwa mfano Juisi ya Tende hii ina matokeo ya haraka kama tatizo lako siyo sugu.
JUISI YA TENDE
Chukua tende kiasi kama robo kilo zitoe kokwa ,weka kwenye blenda,tia maziwa fresh kidogo zisage,na utaongeza maziwa kadri uzito wa juisi utakaohitaji na usitie sukari.
Juisi hii unaweza ukaongeza na unga wa habat sawda, unga wa tangawizi na unga wa karanga au soya kiasi kama kijiko cha chai.
Na kama hauna blenda basi kunywa maziwa fresh na tende,na unaweza ukaongeza na karanga mbichi na kipande cha tangawizi au ukatia unga wa tangawizi katika maziwa ya moto pamoja na Habat sawda ya unga na ukaweka asali.
Pia katika juisi ya tende unaweza ukaweka na asali kidogo.
Na unaweza ukatengeneza mchanganyiko wa Asali,Habat sawda,Tangawizi ya unga,Mdalasini ya unga, Kitunguu sawm (Garlic paste) ukawa unatumia kama jam au ukala vijiko viwili asubuhi na jioni huku ukitafunia na karanga au korosho au Brown bread.
JUISI YA TIKITI MAJI.
Andaa juisi ya tikiti maji bila ya kutoa mbegu, weka jikoni kamulia Limao kidogo na ikianza tu kuchemka itoe jikoni,kunywa.
Hivi ni baadhi ya vyakula vinavyopatikana katika mazingira yetu.Tujitahidi kuvitumia ili kuoberesha afya zetu.
Endapo unajua tayari una upungufu wa nguvu za kiume, tambua kuwa tiba yako siyo vyakula bali unatakiwa kupata tiba kwanza kisha ndipo uanze kutumia hivyo vyakula ili usiweze kurudi kwenye tatizo lako kama mwanzo.
Tunayo dawa iliyotengenezwa kutokana na mimea ya Butea Superba inayopatikana katika nchi ya Thailand pekee. Dawa hii ipo katika mfumo wa vidonge na ni vidonge vinne tu kwa dozi moja. Matumizi yake ni kumeza kidonge kimoja tu kwa siku, hivyo dozi inaisha baada ya siku nne pekee.
Upatikanaji wa dawa hii ni rahisi tu kwani unaweza kuipata direct mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Morogoro, Tanga na Dar es salaam. Mikoa mingine tunatuma kupitia Ofisi za mabasi ya mikoani
Mawasiliano
0784925000
0767925000
0622925000 whatsapp
Sunday, 20 December 2015
WANAWAKE: JE, UNAJUA PED UNAYOTUMIA INA NINI?

Ndugu zangu huwa nawaambia kila siku kitu cha bei chee, sio chakutumia maana ni ADUI WA AFYA YAKO. Huna haja ya kununua ugonjwa ambao utakugharimu mamilion kwa kuepusha pesa ambayo utaenda kuiepusha hata kwenye vitu ambavyo sio vya KUILINDA AFYA YAKO.
Napenda nikwambie kuwa material yanatumika kutengeneza,pedi hizi za mtaani zinatokana na kuchukua mabaki ya karatasi,plastics na kemikali mbali mbali zikapitishwa kwenye machine (RECYCLING) na hatimaye kupata material ya pedi unazotumia.
Ndugu yangu kundi inayotumika kugundishia pedi hizo kwenye nguo ya ndani ili ikae vizuri imetengenezwa kwa kutumia BENZENE! Nenda google andika madhara ya benzene kwa mwanamke utalia
-Inavuruga mzunguko wa kike
-inaharibu mzunguko wa kike kwa kuleta maumivu,kichefu chefu yani kitaalamu (dysmenorhea)
-Pia inaweza,kusababisha kubleed kwa muda mrefu bila sababu yoyote tena ovyo ovyo (Polymetrohagia)
-Pia inasabisha kukosa kabisa hedhi bila hata sababu ya maana (Amenorhea)
Je inatokeaje?
Endapo ukisha toa pedi, kuna chembe chembe za benzene zinaweza baki na kuingia kwenye sehemu mahusisi za uzazi na kusababisha matatizo yote hayo.
Hili ni janga kila dada ana lalamika mzunguko, ugumba,uvimbe kwnye kizazi watoto wadogo tu, yote haya inategemea jinsi gani mwili wako unaitikia kwenye hii benzene. Km upo sensitive utapata mdhara haraka na km hauko sensitive utachelewa kupata madhara.
Sasa napenda kuwaambia we differ genetically how our body responds to environmentall triggers!
Chukua tahadhari mpendwa kuepusha Afya yako.
PED & PANTLINER ZETU
Ped zetu zimetengenezwa Kwa Technologia ya hali ya juu.ped zetu na Pantliner zinetengenezwa Kwa Anion Chip Technology.Anion ni negative particles ambazo zinatoa oxygen pale zinapogusana na mwili wako. Joto la mwili linapokutana na pedi au pantliner inaachia negative particles ambazo mwisho wa siku inatoa hewa safi ya oxygen.
ANIONS Kwa inapatikana kwenye maporomoko ya Maji, chemichemi ya Maji kwenye misitu, Mvua za acidi, Moshi wa misitu baada ya kuunguzwa n.k.
FAIDA ZA ANION CHIP
1. Ina uwezo wa kuondoa muwasho, bacteria, fungus wa aina yoyote kipindi cha Hedhi
2. Inaondoa harufu mbaya
3. Inarekebisha mzunguko na kuweka homoni sawa.
4. Inatibu Ugumba
5. Inaondoa msongo wa mawazo na uchovu
6. Inarekebisha mfumo wa homoni za mwili
7. Pantliners Pia zinatumika na wanaume wenye prostatic hypertrophy, Bawa siri na kutokwa na damu kwenye njia ya haja kubwa
8. Ina uwezo wa kuondoa uvimbe na kuzibua mirija ya uzazi iliyoziba.
9. Inaimarisha kinga ya mwili na kujikinga na matatizo yote ya uzazi.
10. Inaondoa matatizo yote ya uzazi hasa baada ya kuogelea kwenye mabwawa ya kuogelea.
10. Inatibu UTI.
Kwa ujumla Ped zetu na Pantliner zina uwezo Mkubwa wa kutokomeza matatizo yote yanayowakumba wanawake wakiwa kwenye siku zao, Kama kuumwa kichwa, msongo wa mawazo, kuchoka, kuumwa Tumbo, kuwa na flow kubwa na mengine Mengi
0784925000
0767925000
Saturday, 12 December 2015
VYAKULA NA UNENE - SEHEMU YA 5

SEHEMU YA TANO:
LISHE SAHIHI NA JINSI YA KUPANGILIA MLO WAKO
Napenda kusema kwamba ni dhahiri kuwa umekuwa ukitumia kila mbinu uweze kujinasua na uzito mkubwa lakini umekuwa hupati mafanikio yoyote tofauti na kuishia kukata tamaa kabisa. Usikate tamaa kwani nina uhakika umeshindwa kutimiza malengo yako kwa sababu unafikiria kila ushauri wa afya unaoupata unaweza kutimiza malengo yako kumbe sio kweli. Najua umeambiwa kufanya mazoezi, kupunguza kula sana, umekuwa ukiambiwa kuacha kunywa vinywaji vingi vya sukari na vingine vingi vya mfano kama huo lakini umekuwa ukiishia kuongezeka uzito bila hata kupunguza hata kilo moja. Umetumia bidhaa mbalimbali za kupunguza uzito, na umeingia gharama kubwa kwa ajili tu utimize malengo yako, yote hayo ni sahihi ni jinsi gani ulivyo na shauku kubwa ya kuishi na uzito wa kiafya na bila kitambi kabisa.
Mafanikio ya kuishi bila uzito mkubwa na kitambi yapo mikononi mwako rafiki yangu. Kwa sababu ulikuwa hujawahi kusoma na kuelewa ninachoandika basi naomba kuanzia leo anza kufuata hiki ninachotaka kukuambia kupitia kupangilia mlo. Na ili unielewe vizuri kabisa tambua kwamba ushauri wote uliokuwa ukitumia ili kuishi bila uzito mkubwa na kitambi na hukufanikiwa basi ulikuwa na uongo mkubwa ndani yake. Hivyo unatakiwa kuanza kusahau kabisa na kuanza upya safari yako ya kupunguza uzito.
Watu wengi sana nimekuwa nikipokea ujumbe wao wakihitaji japo hata niwaambie wapangilie vyakula gani tangu asubuhi hadi usiku ili waweze kupunguza uzito. Moja ya jibu ambalo wengi nimekuwa nikiwapa ni kurejea kusoma elimu yangu upya kuanzia hatua ya kwanza hadi sasa tulipofika hatua ya sita.
Kama umefuatilia Makala zangu zote basi nina Imani lazima ufikie mafanikio. Ndoto zangu na malengo yangu ni kutaka kuhakikisha kila mtu mwenye kitambi na uzito mkubwa endapo akifuata elimu hii atakuwa shuhuda na daktari katika kizazi chake chote na ukoo wake wote, ndio maana nataka uelewe elimu hii hatua kwa hatua ili uje uwe daktari mzuri wa kitambi na uzito mkubwa katika ukoo wenu na kuondoa fikra potofu kuwa uzito ni moja wapo ya magonjwa ya kurithi na kujisahau kuwa katika familia pia tunarithishana ulaji mbaya wa vyakula na hatimaye kuishia kuwa na uzito mkubwa na kitambi familia nzima kutokana na mwenendo mbaya wa maisha katika familia.
Tangu nianze kufundisha namna gani unaweza kupunguza uzito kiafya,kirahisi kabisa bila gharama yoyote ni kuhakikisha, UNAPUNGUZA VYAKULA VYA WANGA na KULA VYAKULA VYENYE PROTINI YA WASTANI NA VYAKULA VYENYE MAFUTA MAZURI KWA WINGI.
Watu wengi wataguna baada ya kusoma haya kwani sio wewe pekee ambaye umepatwa na hali hiyo kwani wengi hawapendi kufanya uchunguzi na wanapenda kubeba taarifa na kuwa ving’ang’anizi wa kutobadilika.
Miongoni mwa watu walioguna katika aya yangu hapo juu, ndio hao hao ambao hutumia mbinu ya kupunguza uzito kwa kuepuka vinywaji vya sukari na pale pale wanakuwa wanaogopa vyakula vya mafuta vinanenepesha na hatimaye kuishia kupungukiwa viini lishe na kusababisha mwili kutoweza kuendesha shughuli mbalimbali katika kiwango stahiki na hapo ndipo utashangaa mwili wako unavyozidi kunenepa ingawaje unajinyima katika aina fulani ya vyakula. Huku ni kukosa elimu sahihi rafiki! Napenda tu nikumegee kidokezo kuwa unapokula chakula cha wanga gramu moja kitakuja kutumika mwilini mwako na kutoa nishati ya mwili Kalori 4 ambapo unapokula vyakula vya mafuta gramu moja utakuja kupata nishati kalori 9. Unaona rafiki yangu? sayansi hapa ndipo hupotosha fikra za watu! Kwani kwa kawaida sasa ukila vyakula vya mafuta unaweza kusababisha kuhifadhi mafuta! Lakini unapokuja katika swala zima la kuufanya mwili wako kuwa mashine inayounguza mafuta yazingatie haya hapa chini kwani ndio nguzo yako katika zoezi hili unalopenda ufikie malengo kuanzia sasa.
Tafiti zinaonesha kwamba unapokula vyakula vya wanga vina uwezo mkubwa sana wa kupandisha kiwango cha insulin kwenye damu ambayo kazi yake kubwa huwa mbili, Kwanza nataka nikwambie kuwa insulin ni homoni inayotolewa na kongosho ili kuja kuhifadhi sukari iliyozidi katika mfumo wa mafuta na glycogeni. Pili nataka tu tena ujue kuwa insulin inaathiri kupungua kwako uzito inapokuwa katika kiwango kikubwa kwenye damu, kwani inakufanya ujisikie njaa mapema na pia ni homoni inayohifadhi mafuta. Hivyo basi endapo ukihakikisha kiwango cha homoni hii kipo chini muda wote hutaweza kuhifadhi mafuta yoyote tumboni, kiunoni,mgongoni, kifuani,mikononi nk. Njia pekee ya kurekebisha kiwango cha insulin ili kiwe sawa muda wote ni kupunguza kitu kinachosisimua utengenezwaji wake kwa kasi ambapo ni Chakula cha wanga. Hivyo tafiti zimeonesha kwamba watu ambao mlo wao una kiwango kidogo cha wanga huweza kupunguza uzito salama kabisa na bila nguvu zozote.
Lakini sambamba na kupunguza kiwango cha ulaji wa wanga, ili uweze kupunguza uzito zoezi hilo linatakiwa liendane na kuongeza vyakula vya nyuzi sana (Fibers) na vyakula vya protini na mafuta. Endapo ukipunguza wanga katika mlo wako au ukaacha kabisa bila kuongeza kiwango cha mafuta utaishia kupata upungufu wa viini lishe na hatimaye utaongezeka uzito badala ya kupungua. Ndio maana unasoma elimu hii, sitaki ufanye kitu kwa kuambiwa lengo langu nataka utimize malengo yako kwa kusoma na kuelewa na kisha uyaweke katika vitendo utashangaa jinsi gani unavyoshusha uzito wako ndani ya mwezi tu.
Kabla sijagusia mada yangu kiundani Zaidi napenda tu kukuondoa wasiwasi kwani najua umeanza kuwaza sasa, nikiacha kula vyakula vya wanga nitaishi vipi? Ni kweli lazima ujiulize kwa sababu hujawahi kuambiwa elimu sahihi kama hii na inaweza kuwa ni mara yako ya kwanza kusikia, lakini usishangae,Napenda nikupe siri tena katika kupunguza uzito kuna aina kuu mbili ya vyakula vyenye kutoa sukari itokanayo na wanga. Tuna vyakula vyenye kuongeza sukari kwa kiwango kikubwa baada ya kuingia mwilini (High Glycemic Index Foods) na kuna vyakula vyenye kuongeza kiwango kidogo cha sukari baada ya kuingia mwilini (Low Glycemic Index Foods). Mfano wa vyakula vya wanga vyenye kiwango kidogo cha sukari ni viazi vitamu, magimbi,maharage, njegele,matunda mengi, karoti nk kulingana na mazingira ulipo wewe. Pia kuna kundi la kati la aina hii la vyakula ni ngano ambayo haijakobolewa na kundi lenye kutoa sukari nyingi kwenye damu ni ngano nyeupe, popcorn, matunda ni pamoja na tikiti maji,nanasi n.k hivyo vyakula hivi unatakiwa upunguze sana na ndio chanzo kikubwa cha uzito wango kuongezeka kwani inaweza kuwa unakula wanga yenye glycemic index kubwa kila kukicha na ukitegemea kupungua uzito! Najua umeanza kuwaza utakumbukaje na utajuaje kiwango maalumu cha vyakula? Jibu lake ni jepesi sana ndio maana nakushauri utumie mboga za majani kwa wingi na baadhi ya matunda na vyakula vingine vyenye protini na mafuta mazuri kwani ndivyo vyenye kiwango kidogo cha sukari na vyenye kuweza kukufanya mwili wako uache kuhifadhi mafuta na bali uanze kuunguza mafuta.
Basi najua umejifunza kitu, basi kwa sababu unajiuliza sasa utaanzaje safari hii ya kula vyakula sahihi ili uweze kupunguza kitambi hicho na uzito huo, najua kuwa umechoka na uko tayari kuanza safari hii sasa kwani tayari umepata imanivna umefarijika kuwa afya yako sasa inaenda kurudi upya na kuishi maisha ya bila kitambi na uzito mkubwa. Niko tayari kukufanya uyafikie malengo yako kwani dhamira yangu ni kukutimizia ndoto na malengo yako kwa kukupatia elimu sahihi inayozidi kubadili maisha ya watu, sasa ni zamu yako endapo tu ukiwa tayari kuweka katika utekelezaji yote unayosoma katika makala haya.
HEBU, TUANZE NA MFANO WA VYAKULA VITAKAVYOKUWA MLO WAKO KWA MWEZI HUU UKIWA UNATIMIZA NDOTO ZAKO ZA KUISHI BILA KITAMBI NA UZITO MKUBWA.
VITU VYA KUZINGATIA
1. KULA- Samaki, nyama,mboga za majani aina yote,mayai ya kienyeji na Siagi
2. USILE/PUNGUZA- Vyakula wa Sukari na Wanga ( Wali,mikate,chapati,baga,mandazi na jamii zingine zitokanazo na ngano ,tambi,maharage,viazi vitamu na viazi mviringo)
3. Jitahidi kula pale tu unapokuwa una njaa na sio kwa sababu kuna chakula mbele yako, na hakikisha kila unapokuwa una njaa hakikisha umekula hadi kutosheka chakula sahihi.
4. Tafiti zinaonesha kwamba unapopunguza sukari kwa kupunguza vyakula vya sukari na wanga, Unapunguza kiwango cha insulin kwenye damu kinachofanya kazi ya kuhifadhi nishati katika mfumo wa mafuta na matokeo yake mwili utaanza kuunguza mafuta na kuwa mtu wakutosheka na kushiba haraka na kuondokana na tatizo la ulaji hovyo kuliko kuwa kunasababishwa na kiwango kikubwa cha insulin kwa sababu ya ulaji mbovu.
Baada ya kupata somo kwa ufupi haya basi tusome kwa undani kabisa hapa chini
1. ULAJI WA NYAMA
Kumbuka maada yangu ya aina za mafuta ya protini katika somo langu la sehemu ya tano. Nyama ina protini na pia ina mafuta. Hivyo kama unahitaji kupunguza uzito nakukubalia kabisa katika mlo wako kuweka aina yoyote ya nyama kwani utajipatia aina kuu hizo mbili za viini lishe vikubwa. Kula nyama ya Ng’ombe,mbuzi,kondoo,kuku,wanyama pori,bata nk unaruhusiwa kula aina yoyote ya nyama.
2. SAMAKI
Unaruhusiwa kula samaki wa aina yoyote kwani samaki wana kiwango kingi sana cha mafuta mazuri ambayo huongeza Omega 3 katika mwili wako ambayo kazi kubwa ni kulainisha mishipa na kufanya mzunguko wa damu ufanye kazi katika ufanisi wa hali ya juu kiafya. Kula sangara, sato, samaki wa baharini nk
3. MAYAI
Unatakiwa ujue kuwa mayai ni chanzo kizuri sana cha viini lishe vikuu kama mafuta na protini. Hivyo unaweza kutumia mayai ya kuchemsha au kukaanga na mafuta ya alizeti/olive oil.
4. MBOGA ZA MAJANI ZINAZOSTAWI JUU YA ARDHI
Mboga za majani zina kiwango kingi sana cha nyuzi (fibers) na hivyo zitakufanya muda wote tumbo lako liwe limeshiba na kiwango cha insulin kuwa katika usawa muda wote. Mbali na hivyo utajipatia madini kama manganese, selenium ambayo ni vionjo vinavyosaidia shughuli za mwili zifanyike katika kiwango stahiki na mwili kuweza kuunguza mafuta.
Mfano
-Kabeji
-Spinachi
-sukuma wiki
-Brokoli
-Cauliflower
-Bilinganya
-Uyoga
-Tango
-Vitunguu
-Pilipili
-Asparagus
- Zucchini nk
5. MATUNDA
Usipendelee sana kula matunda kwa sababu matunda, unapokuwa umekula angalau matano kwa siku ni sawa kama umekunywa soda milimeta 500. Hivyo jitahidi kuepuka. Na kama unahitaji kutumia kama juisi hakikisha unatumia blenda ambayo inaitwa (Centrifugal juicer) hii inakuwa na sahani katikati ambacho huzunguka na kupiga kelele. Aina hii ya blenda inakufaa sana kwa wewe unayetaka kupunguza uzito ila hakikisha juisi yako umekunywa ndani ya dakika 15 kwa sababu baada ya dakika hizo vitamin zitakuwa sio hai tena kwa sababu ya mwanga na joto wakati wa kusaga juisi yako. Blenda hii pia huacha nyuzi nyingi sana na hivyo inafaa kwa wewe unayetaka kutimiza malengo yako, Epuka juisi zile cold press juicer ambazo hukamua juisi bila sauti yoyote na inaondoa nyuzi zote itakufanya kuongezeka uzito wako kwa kasi sana maana kutakuwa na sukari nyingi.
Nakushauri glasi moja asubuhi na jioni ya juisi inatosha.
Tumia matunda kama Apple, Parachichi nk
6. Mafuta kwa ajili ya matumizi yako.
Jitahidi utumie mafuta kama Olive oil, alizeti katika kuandaa mlo wako
MFANO NAMNA UNAVYOWEZA KUPANGIA VYAKULA HAPO JUU
Mfano
ASUBUHI UNAPOTAKA KWENDA KAZINI
-Chukua supu yako ya kuku wa kienyeji,kachumbari ya parachichi,tango,kitunguu maji,pilipili hoho. Baada ya nusu saa kunywa maji ya baridi kwa mbali sana. Utajiskia kushiba kuzidi hata yule anayekula vyakula hatari kama chapatti,mandazi,tambi angali bado ana uzito mkubwa
SNACK (KATIKATI YA ASUBUHI NA MCHANA)
Endapo ukijiskia mwenye njaa, Chukua yai lako moja lililochemshwa shushia na maziwa asili ya ng’ombe( Epuka maziwa ya kiwandani namaanisha yaliyohifadhiwa kwenye box). Utajisikia mwenye kushiba na kuridhika na ulicho kula. Mwili wako utakuwa wenye nguvu na utakaa muda mrefu bila njaa kabisa kwani kiwango cha homoni ya insulin kiko chini ya kiwango, kuliko ungelinunua kinywaji chenye sukari kama soda ambacho kinahatarisha maisha yako na uzito wako.
MCHANA
Chukua Mboga kama Brocolli chemsha kwa mvuke kisha kata kata kama kachumbari, unaweza kuchanganya na matunda mengine yoyote kama unayo. Unaweza kuchanganya na mchemsho wa samaki. Kisha kula utajisikia umeshiba kuliko yule angeagiza chakula ambacho ni wali, ndizi, pilau, chips, mtoli n.k, huu ni ulaji wa bila kujali afya yako kwani unakula kama vile hufikirii mstakabali wa afya yako na inaonesha umekata tamaa kwa sababu huwezi kula mlo ambao watu ambao hawana kitambi,uzito mkubwa na kisukari wanatumia na wewe utumie. Jitahidi kuepuka vyakula ambavyo vinaweza kutokutimizia malengo yako
USIKU
Pia unaweza kuwa mbunifu wewe mwenyewe kulingana na radha ya chakula unayoitaka. Unaweza kukaanga yai lako moja kwa mafuta ya olive, changanya na kachumbari ya mboga za majani na matunda yasiyokuwa na chachu kama parachichi na tango usisahau kuweka natural antibiotic pilipili kwa mbali. Kisha shushia na maziwa yako ambayo ni ya asili(Organic whole milk)
NOTE: Wengi mnapotaka kupunguza uzito MCHANA Binafsi huu mfumo una uzuri wake na ubora wake lakini ningekushauri kuwa kama unataka kupunguza uzito nimesema mwanzo HAKIKISHA UNAKULA CHAKULA PALE TU UNAPOKUWA UNAJISKIA NJAA NA TUMBO HALINA KITU NA EPUKA KUJINYIMA KULA MAANA KUNAONGEZA UZITO KWA KASI SANA. Hivyo itapendeza usipofuata saa yako kuwa unakula pale tu familia yako inapoivisha chakula, sivyo! Kula chakula pale tu unapokuwa una njaa hii itapunguza ulaji usio na msingi kwa kisingizio chakula kipo mbele yako.
Napenda kusema asante kwa mnaoendelea kufuatilia maada zangu.
Njia pekee ya kupunguza uzito ni kupata ELIMU SAHIHI YA LISHE.
NAPENDA KUCHUKUA NAFASI HII KUKUOMBA KUSHARE,POST HII POPOTE PALE UTAKAPO ILI KUWEZA KUWAPASHA HABARI WATU WENGI NA WAUNGANE NASI KATIKA JUKWAA HILI LA ELIMU YA LISHE .
Masha
0784925000
0767925000
0622925000 whatsapp

