Sunday, 10 July 2016

HATUA 5 ZA KUPATA MTOTO WA KIUME




Kupata mtoto wa kiume ni jambo linalohitaji ushirikiano wa pande zote mbili, yaani mke na mume na ni jambo linalohitaji hatua kwa hatua na kwa umakini, ingawa njia nitakayoeleza hapa haimaanishi kuwa inaweza kufanya kazi kwa asilimia 100.  Bali ni njia ambayo imekuwa ikitumika mara kwa mara na ndiyo njia rahisi na ukiifuata unaweza ukapata kwa asilimia 75.

Mwaka 1960 mwanasayansi Landrum Shettles aliandika kitabu kinachohusu uchaguzi wa jinsi ya mtoto.  Mwanasayansi huyo wa tiba ndiye aliyeileta nadharia yake iliyojikita zaidi katika vitu vilivyomo ndani ya seli, yaani malighafi za kijenetiki ziitwazo chromosomes ambayo ndiyo inayotumika na kama ikifuatwa vizuri basi huweza kuwa na mafanikio.

Sayansi ya kijenetiki inaeleza kuwa mwanamke huwa na mbegu ya XX na wa kiume huwa na XY, na pale yai la kike linaporutubishwa hutokea mgawanyiko wa seli na mbadilishano wa malighafi za kijenetiki hutokea.

Hivyo kiumbe kinachotungwa yaani mtoto, huwa na nusu ya malighafi za kijenetiki kutoka kwa mama na nusu nyingine kutoka kwa baba, na akipata mbegu XX huwa ni jinsi ya kike na akipata XY ni wa kiume.
Kiasilia mbegu Y huwa ni ndogo kimaumbo, zina mwendokasi mkubwa lakini hufa mapema ukilinganisha na za kike X ni kubwa, hazina kasi, lakini huishi kwa muda mrefu.  Kwa kutumia ufahamu huu ndipo mwanasayansi Shettels aliweka nadharia ambazo zinatumika katika uchaguzi wa jinsia.

Kuna hatua tano za kufuata kwa umakini ili uweze kufanikiwa, ingawa haimaanishi kuwa ni lazima ufanikiwe kwani hatua hizi huongeza nafasi zaidi ya kupata jinsi ya kiume na kwa yule atakayehitaji jinsi ya kike afanye kinyume cha hatua hizi.

Hatua ya kwanza
Hatua ya kwanza ni kugundua wakati wa ovulation, ama siku ambayo yai la kike linatoka.  Hiki ni kipindi ambacho yai la mwanamke lipo tayari kurutubishwa na mbegu ya kiume hivyo mimba huweza kutungishwa.

Ili kugundua kuwa upo katika ovulation, inabidi kufuatilia yafuatayo: Inabidi uwe na chati ya kuangalia na kufuatilia ute wa kizazi unaotoka ukeni, maana muda mfupi kabla ya ovulation ute huwa wa majimaji na wa kuvutika hufanana kama vile wa mayai ya kawaida, nikimaanisha ya kuku, ambayo yamezoeleka kwa wengi.

Ni vizuri kupanga chati hii kwa zaidi ya miezi mitatu ili kusudi uwe na uzoefu wa kugundua tofauti ya ute.  Vilevile inabidi uwe na chati ya kuweka rekodi ya joto la chini la mwili wakati ukiwa umepumzika, nikiwa na maana mara nyingi ukiwa umelala.

Joto la chini la mwili hupanda kwa nyuzi joto 0.5 sentigredi kipindi cha ovulation.  Ni vizuri chati hii iwe pamoja na ya ute wa kizazi, kusudi uweze kufuatilia mabadiliko haya kwa pamoja.

Kipimo cha kugundua ovulation ni kipimo ambacho huangalia wingi wa homoni aina ya Lutenizing ambayo hutolewa kwa wingi kipindi hiki.  Kipimo hiki ni vizuri kufanya mara mbili kwa siku, kati ya saa 5:00 asubuhi na saa 9:00 mchana.  Vilevile kati ya saa 11:00 jioni na saa 4:00 usiku.

Hatua ya pili
Hii ni hatua ya kutegea wakati muafaka wa kufanya tendo la ndoa.  Ni vizuri kufanya tendo la ndoa kipindi cha saa 24 kabla ya ovulation na saa 12 baada ya ovulation.  Kwa sababu tindikali na utelezi katika ute wa kizazi hupungua na hivyo husaidia mbegu za mwanaume hasa aina ya Y kusafiri haraka na kulifikia yai la mwanamke na kulirutubisha.

Hatua ya tatu
Pendelea mtindo au staili inayofanywa na wanyama kama mbuzi wakati wa tendo la ndoa, yaani mtindo wa mwenza wako kuinama.
Mtindo huu huwezesha mlango wa uzazi kuwa karibu na sehemu ya kiume pia kuingia umbali mrefu zaidi ndani ya uke, hivyo basi mbegu za kiume humwagwa karibu na shingo ya kizazi na kulifikia yai haraka zaidi.

Hatua ya nne
Ni muhimu mwanamke kufika kileleni kabla ya mwanaume; kufika kileleni kwa mwanamke husaidia kubadili mazingira katika uke kuwa ya ukakasi (alkaline) hivyo kusaidia mbegu za kiume “Y” kuwa imara zaidi.  Uke kuwa na tindikali huipunguza uimara wa mbegu ya kiume.

Hatua ya tano
Hii ni kwa upande wa mwanaume.  Ni vizuri kuvaa nguo zisizoweka joto kali na kubana.  Unapaswa kuvaa chupi au nguo ambazo hupwaya na zimetengenezwa kwa pamba.  Nguo za ndani zinazobana ambazo huongeza joto hupunguza idadi ya mbegu za kiume.  Joto pia hupunguza ubora na utengenezaji wa mbegu za kiume.

Vilevile inabidi kunywa vinywaji vyenye caffeine kabla ya tendo la ndoa.  Hii huongeza nguvu ya mbegu za kiume aina ya Y.

Mambo mengine ya kuzingatia ni mlo.  Hakikisha unakula vizuri wiki moja kabla na siku ya tendo.  Tafiti zinaonyesha kuwa ulaji wa vyakula vyenye sukari huiwezesha mbegu ya Y kuimarika zaidi na kuongeza nafasi ya kupata mtoto wa kiume.  Vyakula hivi ni kama matunda matamu, vyakula vya wanga na vinywaji vyenye glukosi.

Vyakula vingine ni kama vile nyama nyekundu, mayai, maziwa, vyakula vya baharini kama vile samaki, kamba na pweza.

Kwa upande wa mwanamke, anapaswa kula zaidi vyakula visivyo na tindikali kama vile kuepuka kula matunda yenye uchachu na vyakula jamii ya kunde kupitia kiasi.

Mambo mengine ni kuzingatia mazingira ya tendo lenyewe, hakikisha upo vizuri kiafya, kimwili na kiakili.  Usiwe na msongo wa mawazo na sonona kwa sababu huleta mwingiliano na tendo, hivyo kulifanya kuwa dhaifu.


Ni vyema pia kutafuta mazingira mazuri ya kufanyika kwa tendo lenyewe.  Lengo ni kuwa na utulivu wa kimwili na kiakili pia.  Hii itakuepusha pia na usumbufu utakaoweza kuleta mwingiliano na tendo lenyewe

FAHAMU KUHUSU TATIZO SUGU LA CHUNUSI

chunusi ni nini? 
hivi ni vipele vinavyotokea usoni, kifuani na mgongoni sababu ya kubadilika kwa mfumo wa kutengeneza mafuta wa ngozi.

chanzo ni nini?
hii husababishwa na kuongezeka hormone za uzazi aina ya testosterone kwa jinsia zote hasa hasa kipindi cha kubalehe na kuvunja ungo kwa jinsia zote.

matibabu.
matibabu yamegawanyika katika sehemu kuu tatu kama ifuatavyo....matibabu kwa chakula, matibabu ya kimwili na matibabu ya dawa za hospitali.


matibabu ya chakula..

  •  ondoa chumvi kwenye chakula chako au kula chumvi kidogo sana.
  •  epuka ulaji wa sukari na vyakula vyote vya kukaanga kama chips, maandazi na chapati.           
  • pendelea kula vyakula vya asili kama wali, ugali, mchicha, maharage, njegere vikiwa vimeungwa mafuta kidogo sana  pia kula kwa wingi karoti mbichi kwa sababu zina vitamin A ambayo ni nzuri sana kwa ngozi
  • kunywa maji mengi ili kuondoa sumu zote mwilini na kulainisha ngozi.

matibabu ya  kimwili.

  •  acha ngozi yako ipate jua la asubuhi na jioni kila siku.
  • weka sura yako kwenye mvuke wa maji ya moto kila siku. 
  • shiriki mazoezi ya aina yeyote hata kama ni kuruka kamba tu angalau utokwe jasho kupunguza kiasi cha mafuta mwilini.                                                                                                                                          
 matibabu ya dawa

  • kuna dawa zinasaidia kuondoa chunusi i.e antibiotiki kama doxcycline, vidonge vya vitamini A na vidonge vya hormone kwa wanawake mfano oetrogen, persol tube na kadhalika. 

 mwisho:
 watu wengi hawaponi chunusi kwa sababu ya kupenda  kutumia njia moja tu ya matibabu {dawa}, ni vizuri kuchanganya njia zote hapo juu kwa matokeo mazuri na inaposhindikana ni vizuri kumuona daktari bingwa wa ngozi kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

Uvimbe sehemu ya haja kubwa - bawasiri/bawasili (HAEMORRHOIDS)



Bawasiri ni mojawapo ya tatizo ambalo mara nyingi linapotokea humfanya mtu kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba sahihi. Bawasiri au hemorrhoids husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.
Kuna aina mbili za Bawasiri
Nje: Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa, na huweza kuambatana na maumivu, pamoja na kuwashwa kwa ngozi katika eneo hilo. Mara nyingine mishipa hiyo ya damu (vena) hupasuka na damu huganda na kusababisha aina kitaalamu inaitwa Thrombosed hemorrhoid.
Ndani: Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa. Na huwa haimbatani na maumivu na wengi huwa hawatambui kuwa wanatatizo hili.
Aina hii imegawanyika katika mainisho yafuatayo:
  • Daraja I- Bawasiri kutotoka katika mahali pake pa kawaida
  • Daraja II- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya tukio hilo.
  • Daraja III- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kuirudisha mwenyewe baada ya tukio hilo.
  • Daraja IV- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na vigumu mtu kuirudisha baada ya tukio hilo.
                 
Je bawasiri husababishwa na nini?
Bawasiri husababishwa na;
  • Tatizo sugu la kuharisha
  • Kupata kinyesi kigumu
  • Ujauzito
  • Uzito kupita kiasi (obesity)
  • Kupenda kufanya ngono ya njia ya haja kubwa (anal sex)
  • Kwa ujumla mambo yanayoongeza shinikizo katika tumbo.
  • Umri mkubwa
Dalili za bawasiri
  • Damu kunuka kinyesi wakati wa kujisaidia (hematochezia)
  • Maumivu au usumbufu
  • Kinyesi kuvuja
  • Kijiuvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
  • Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
  • Kujitokeza kwa kinyama (bawasiri) wakati wa haja kubwa
Matatizo yanayoweza kutokana na Bawasiri
  • Upungufu wa damu mwilini (Anemia)
  • Strangulated hemorrhoids
Vipimo na uchunguzi
  • Digital rectal examination
  • Kipimo cha njia ya haja kubwa (Proctoscope)
  • Kipimo cha utumbo mpana (Sigmoidoscope)
Matibabu
Matibabu hutegemea na hali na aina ya Bawasiri
  • Rubber band ligation - Hapa mishipa hufungwa na rubber band ili kuzuia damu kwenda kwenye eneo liloathirika, na hutumika kwenye aina ya ndani ya bawasiri.
  • Sclerotherapy- Hapa kemikali huwekwa kwa njia ya sindano
  • Coagulation (infrared, laser and bipolar)
Upasuaji;
  • Hemorrhoidectomy
  • Stapled hemorrhoidopexy
Njia za kuzuia Bawasiri
  • High fibre diet, kula mboga za majani, matunda, na nafaka kwa wingi.
  • Kunywa maji mengi kwa siku (glasi sita hadi nane kwa siku)
  • Punguza kukaa kwa muda mrefu sana hasa ukiwa chooni, kwa sababu unaweza kuongeza shinikizo katika mfereji wa haja kubwa.
Njia zingine za kuzuia Bawasiri
1. Jaribu kunywa maji ya kutosha na kula chakula chenye fiber nyingi ili uepuke kupata Choo kigumu.
2. Epuka kusimama muda mrefu au kukaa muda mrefu kama ulikuwa unafanya hivo awali
3. Fanya mazoezi ili kuongeza intenstine motility
4. Epuka kujikamua sana ukipatwa na haja kubwa
NB: Huu ugonjwa hauhusiani na matatizo ya uzazi
Baadhi ya sababu zinazopelekea hali hiyo ni

-kufunga choo ama kupata choo ngumu 
-ujauzito
-sababu za kiurithi-baadhi ya watu wanaweza kuwa na kuta dhaifu

Njia sahihi ya kupunguza Kitambi na Unene



Mtindo wa maisha, vyakula na shughuli za kila siku za mwanadamu ni baadhi ya vitu vinavyosababisha idadi kubwa ya wake kwa waume kuwa na uzito au unene kupita kiasi na wakati mwingine kuwa na vitambi.
Matatizo haya yamekuwa yakiwapata watu wa jinsia zote na kuwanyima raha wanawake wengi, ambao hufikia hatua ya kutumia mikanda maalumu ya kufunga tumbo au kuhangaika kupitia njia mbalimbali ili kupunguza kadhia hiyo kwao.

Kutokana na kuongezeka kwa tatizo hilo, kumezuka dawa nyingi zinazodaiwa kuwa na uwezo wa kupunguza vitambi na uzito mkubwa, lakini wataalamu wa afya wanaonya kuwa ni sumu.

Tafiti nyingi za kisayansi zinaonesha kuwa dawa hizi kwa kiasi kikubwa zina kemikali kama vile phentermine, sibutramine, phenolphthalein, caffein, hydroxycitric acid (HCA) na senna ambazo zina madhara makubwa kwa afya ya mwanadamu.
Dk. Phil McGraw anasema baadhi ya dawa hizo huathiri sehemu ya ubongo inayohusika na hamu ya chakula.  "Hamu ya chakula ni muhimu kwa ajili ya ubora wa afya na maisha.  Dawa yoyote inayoharibu hamu ya chakula kwa kipindi kirefu, inaweza kusababisha madhara ya kiafya", anasema Dk. Phil.
Mama mwenye uzito wa kilo 108, Doreen Shayo anasema amewahi kujaribu dawa za kupunguza mwili, lakini akapatwa na homa kali iliyohatarisha maisha yake baada ya wiki moja, hivyo alishindwa kuendelea na dozi hiyo.

"Nilishawishiwa kununua dawa hiyo ya kupunguza uzito na nilishauriwa kula mbogamboga, matunda na maji kwa wingi wakati wa dozi, sikuwa nakula wanga wala chakula kamili.  Nilipata homa ya ghafla madaktari wakanishauri kwamba dawa zile hazikuwa nzuri kwangu hivyo niachane nazo, wakati huo nilikuwa na kilo 120 lakini nilipungua kutokana na maelekezo ya madaktari", anasema Doreen.
Baadhi ya madaktari bingwa wa afya ya binadamu wanasema msukumo wa dawa hizo unaowafanya wahusika kuharisha mafuta mengi kwa wakati mmoja, ni njia isiyo sahihi ambayo pia huathiri baadhi ya viungo ndani ya tumbo, huku madhara yake yakijitokeza miaka kadhaa mbeleni.

Tabibu mmoja wa tiba mbadala anasema asilimia kubwa ya dawa za kupunguza kitambi na mwili kwa uharaka ni sumu.
"Mtu anapewa dawa anaharisha sana, swali la kujiuliza nini dawa inafanya tumboni na kusababisha kupata choo laini au kuyeyusha mafuta kwa muda mfupi?  Lazima tujue kwamba zina madhara baada ya muda, wengi wanauziwa vitu vibaya na mbegu fulani ambazo ni sumu halafu mwili unabadilika anaharisha sana, anaambiwa dawa ndio inafanya kazi yanatoka mafuta mengi, si njia sahihi ya kupunguza uzito wa mwili au kitambi."

Dk. Samuel Shita kutoka Hospitali ya Mwananyamala anasema kwa kawaida kuharisha humfanya mtu kupunguza maji mengi na chumvichumvi mwilini na hivyo huathiri kazi ya seli na mfumo wa fahamu.

"Dawa hizo nyingi hazijaruhusiwa kutumika na Wizara ya Afya na wala hazijathibitika kwamba ni sahihi kwa matumizi ya binadamu, lakini wanazitumia na madhara yake yanaanza kujitokeza baada ya kutumia mtu anaharisha sana na yeye anadhani ana mafuta lakini ule ni uteute unaokaa tumboni unaosaidia tumbo kufanya kazi.

"Utafiti unaonesha kuwa watu wanaopendelea kula katika migahawa mikubwa ndio wanaoongoza kuwa na miili mikubwa, teknolojia zipo na dawa zitumikazo lazima ziwe zimefanyiwa utafiti kwa zaidi ya miaka 10.  Kuna madhara mengi yanayoweza kuwakuta watu ikiwamo ya figo, moyo, ini na mishipa ya damu."


Dk Shita anasema kuna njia sahihi za kupunguza tumbo ambazo pia ni salama.  "Mtu anatakiwa kufanya mazoezi mepesi na matumizi sahihi ya vyakula, tunatakiwa kupunguza vyakula vya wanga kupita kiasi, sukari na mafuta.
Anasema soda, pipi na chocolate ni vyakula ambavyo havitakiwi kutumika kupita kiasi.

Tabibu wa tiba mbadala anazitaja hatua sahihi za kupunguza kitambi na kuondoa sumu mwilini akisema: "Kutumia juisi za matango na nyanya kila siku kwa muda wa mwezi mmoja sumu zote zinaondoka."
Hata hivyo, Mwaka anasema mtu anapokula chakula ni lazima kiishe tumboni kabla ya kuingiza kingine, vinginevyo anakuwa ametunza sumu mwilini kutokana na kuwa na mabaki mengi ya chakula cha takriban hata mwaka mmoja.

"Mfuko wa chakula una uwezo wa kutunza chakula kwa muda mrefu, ndiyo maana binadamu hufa akikosa chakula kwa siku nyingi.  Miongoni mwa vitu vinavyofanya uondoe sumu mwilini ni kufuata sheria za ulaji na njia za asili za kuondoa sumu hiyo na si njia za haraka kwani zina madhara," alisema.
Wataalamu wa masuala ya dawa Deborah Mitchel na David Dadson, katika kitabu chao kilichochapishwa mwaka 2002 cha "The Diet Pill Guide: The Consumer's Book of Over-the-Counter and Prescription Weight -Loss Pills and Supplements," wanasema:

"Ingawa ushahidi wa dawa hizi unazidi kuongezeka, bado watu wengi wanaaminishwa kwa uongo kuwa zina manufaa.  Hata hivyo, pia watu wanaendelea kuamini kuwa dawa hizi zinazotokana na mimea na ni dawa salama za asili zinazofanyiwa utafiti wa kina na kuthibitishwa na mamlaka za udhibiti na usalama wa dawa kama nyingine za hospitalini."

Namna ya kupunguza kitambi


Maji ya moto yakitumiwa kwa umakini yana uwezo wa kupunguza kitambi, tumbo au uzito mkubwa wa mwili kwa asilimia 60.
"Maji ya moto yana uwezo wa kupunguza tumbo kwa zaidi ya asilimia 60, unachotakiwa kufanya ni kuyachemsha yawe ya vuguvugu kiasi kunywa kati ya glasi nne mpaka sita na iwe ni katikati ya mlo mpaka mlo ndiyo maana kuna watu wanashauri unywe asubuhi au iwe katikati ya mlo wa jana usiku na ule utakaokwenda kuula baadaye.

"Lakini pagumu zaidi ni pale ambako kabla hujakwenda kupiga mswaki ndiyo unatakiwa kuyanywa haya maji.  Tunapata vitamin B12 ambazo zinazalishwa mdomoni wakati binadamu akiwa amelala na mojawapo ya vitamin hiyo ni pamoja na kusaidia msagiko (mmeng'enyo) ule wa vyakula."

Tatizo la wengi kukaa na vyakula kwa muda mrefu tumboni ni moja ya sababu pia ya kuwa na tumbo kubwa yaani kuwa na mafuta ya ziada tumboni na wengine wanakuwa na vyakula vingi wanavyoingiza kuliko wanavyovitoa.



"Asubuhi kabla hujapiga mswaki ukaondoa zile vitamin mdomoni zinywe pamoja na maji, kunywa maji ya vuguvugu glasi nne mpaka sita kila siku unapoamka asubuhi mfululizo mpaka siku 21, baada ya muda fanya hivyo kwa wakati mwingine na wakati ukifanya hivyo pia epuka vile vitu vitakufanya uendelee kuwa na tumbo ili unachokifanya kiweze kuwa na majibu na si kuoga na kujipaka tope," anasema na kuongeza kuwa kupunguza vyakula vya wanga ni njia mojawapo itakayomfanya mhusika kupata majibu ya haraka

MAUMIVU MAKALI YA MGONGO


UTANGULIZI

Maumivu ya mgongo ni ile hali ya kuhisi maumivu au kutojiskia vizuri/kawaida katika misuli au mifupa ya mgongo wako (eneo lililopo kati ya kiuno na shingo).

(Mgongo)
Maumivu haya yanatofautiana baina ya mtu na mtu na pia yanategemea sana wapi ilipo shida katika mgongo wako; nini kisababishi na kiungo kilichoathiriwa (kilichoumizwa/jeruhiwa).

Vivyo hivyo dalili nazo hutegemea na kisababishi na hivyo baadhi ya watu huwa na dalili zinazofanana huku wengine wakiwa na dalili za aina mbalimbali kuanzia maumivu ya mgongo, kushindwa kufanya shughuli za kawaida za kila siku kutokana na maumivu, homa na kutetemeka, kupungua uzito (hasa baada ya ajali/magonjwa ya mifupa), kupungua nguvu katika misuli ya miguu, miguu kuwaka moto/kuchomwa chomwa mithili ya sindano au miiba, ganzi kwenye miguu hadi kushindwa kumudu kuzuia haja ndogo na/au kubwa.

Aina kuu za maumivu ya mgongo:
Mara nyingi, maumivu ya mgongo hujitokeza katika aina kuu mbili ambayo ni:
(Maumivu yanayosambaa)
  1. Maumivu yasiyohama (yapo katika eneo la mgongo husika haijalishi unafanya nini - localized pain). Mara nyingi maumivu ya namna hii ni yale yanayokuwa yametokana na kujeruhiwa kwa misuli/mifupa ya mgongo kwa ajali au kupigwa eneo la mgongoni. Au, ni yale yanayotokana na mkao mbaya usiozingatia afya ya mgongo hivyo kusababisha kuchanika kwa misuli ya ndani ya mgongo na kusababisha maumivu!!
  2. Maumivu yanayosambaaa na kuangazia maeneo mengine ya mwili wako mbali na mgongo kama vile miguu. Maumivu haya hutokana na mgandamizo katika mfumo wa fahamu/neva kutoka kwenye mifupa, uvimbe au kuumizwa kwa uti wa mgongo/neva zinazochomozea mgongoni baada ya ajali au kujeruhiwa mgongo wako kwa kupigwa/kuanguka. Mfano: shida ipo mgongoni ila unahisi ganzi kwenye miguu au miguu kuwaka moto).


Visababishi vya maumivu ya mgongo:
(Ubebaji wa mizigo)
  1. Moja ya visababishi vikuu vya maumivu ya mgongo ni aina ya kazi unayofanya. Kazi inayohitaji muda mwingi katika kukaa/kusimama au unaifanya ukiwa katika mkao wa kuinama ni kichocheo cha kupata maumivu ya mgongo.
  2. Mkao: nyumbani, kazini, shuleni, n.k wakati unafanya shughuli zako za kila siku, una nafasi kubwa katika kuongeza au kupunguza hatari ya kupata maumivu ya mgongo
  3. Ubebaji wa mizigo mizito (kufikia kilo 5 au zaidi) usiozingatia afya ya mgongo.
  4. Kulalia godoro laini na lililobonyea/linalobonyea katikati wakati wa kulaa. Hii husababisha misuli ya mgongo kuvutika kupita kiasi wakati umelala na kupelekea kuchanika hivyo kuishia
    (Godoro la kubonyea)
    katika kupata maumivu ya mgongo na ambayo hudumu kwa muda mrefu (wote) utakokuwa unalalia
      godoro hilo au hata zaidi.
  5. Kujeruhi(wa) mgongo wako kunakotokana na ajali, michezo, kuanguka, kupigwa, n.k au uvimbe (kansa) katika uti wa mgongo.
  6. Ujauzito/uzito wa kupita kiasi (kitambi): wengi wanashtuka wanaposikia kuwa uzito (kitambi) husababisha maumivu ya mgongo, ila akina mama wajawazito wanafahamu! Kinachotokea huwa ni kubadilika kwa mfumo mzima wa maumbile ya mgongo na hivyo kusababisha baadhi ya misuli/mifupa kubeba uzito wakati wa kukaa au kusimam. Kuelemewa kwa misuli/mfupa hii husababisha mabadliko ya mwili katika kutafuta namna ya kufidia hali hiyo… mwisho ni maumivu!!!
  7. Msongo wa mawazo (stress): msongo wa mawazo humfanya mtu kukaa katika mkao mbaya akiwaza na kuwazua hivyo kuishia katika kupata maumivu ya mgongo
    kama nilvyotangulia kusema hapo juu.
  8. Magonjwa yanayoathiri mifupa (pingili) za mgongo kama vile TB ya mifupa ya mgongo na misuli ya pembeni mwa mifupa hiyo na kusababisha maumivu katika eneo husika.
  9. Kuvunjika au kuhama kwa mifupa ya mgongo kutoka nafasi yake ya hapo awali kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo ajali.
    (Msongo wa mawazo)
  10. Umri wa uzeeni: kadri mtu anavyozidi kuukaribia uzee ndivyo kunavyozidi kutokea mabdiliko katika mifumo yote ya mwili ikiwemo ile ya mifupa-na-misuli hivyo kuleta matatizo mengine ya kimfumo yakiwemo maumivu ya mgongo na mengineyo.[Wanawake huathiriwa mapema katika uzee wao kuliko wanaume kutokana na mfumo wa vichocheo (homoni) vya miili yao kupungua kwa haraka zaidi baada ya miaka kati ya 45-55 ya umri wao wa kuishi).
  11. Wanaume kujihusisha na UPIGAJI PUNYETO wakati wa ujana wao. Vijana wengi ukiwauliza watakwambia wameufanya sana mchezo huu na hadi wengine kufikia kuuhalalisha kuwa ni kawaida kufanya hivyo. Kitendo hiki huhusisha kwa sana uti wa mgongo na ubongo hivyo ni chanzo kimojawapo cha maumivu ya mgongo na hata upungufu wa NGUVU ZA KIUME


Matibabu:
  • Mumivu ya kwaida hasa yale yanayotokana na mshtuko wa misuli ya mgongo au mkao mbaya huwa yanaisha yenyewe ndani ya siku 4 -14, hivo mgonjwa anashauriwa kutumia dawa za kawaida za kutuliza mamivu.
  • Maumivu yanayotokana na kujeruhiwa mgongo ikiwa ni pamoja na ajali/kupigwa/kuangukia mgongo n.k) unashauriwa kufika hospitalini au kituo cha afya kilicho karibu nawe ili upate uchunguzi yakinifu na ushauri/tiba.
  • Maumivu yanayoamabatana na kushindwa kumudu kuzuia haja ndogo na/au kubwa, maumivu makali ya miguu, miguu kuwaka moto/ganzi yanahitaji tiba ya haraka na dharura kwa sababu tayari mfumo wa fahamu/neva utakuwa ulishaguswa/athiriwa kwa namna moja au nyingine.


Namna ya kuzuia maumivu ya mgongo:

(Namna ya kunyenyua mzigo)
  • Mwone daktari wa tiba viungo (PHYSIOTHERAPIST) aliye karibu nawe kwa ushauri kuhusu namna ya:
  • Kukaa vizuri ukiwa nyumbani, kazini au shuleni 
  • Namna ya kubeba mizigo kwa kujali na kuingatia afya ya mgongo wako ili kuepusha kujeruhi misuli ya mgongo wako.
  • Mpangilio na uboreshaji wa mazingira ya kazi yako ili kuzuia hatari za kupata maumivu ya kimfumo (misuli-na-mifupa)
  • Mazoezi muhimu kwa ajili ya afya ya mgongo wako.
  • Tiba ya mazoezi ya viungo (na mgongo kwa ujumla) inayoendana na shida yako husika.

***Kumbuka, tiba ya mtu mmoja mmoja hutaofautiana kwa kuwa dalili hutofautiana kutokana na kisababishi cha maumivu hayo***

***Usifanye mazoezi uliyoona mwenzako akifanya ukidhani unajitibu kumbe ukawa unaongeza tatizo badala ya kupunguza. Ni vizuri umwone mtaalam akuelekeze tiba stahiki***

NJIA SALAMA ZA KUPUNGUZA UZITO


Ukizungumza na watu wengi wanene watakwambia wanataka kujua njia ya kupunguza mafuta tumboni. 
Njia rahisi na salama ya kupunguza mafuta katika tumbo au kitambi ni ile ya kupangilia chakula na kufanya mazoezi.

Kama unataka kupunguza tumbo kwa haraka basi punguza kula vyakula vyenye wanga na badala yake tumia mbogamboga na matunda kwa wingi.

Vyakula kama viazi mviringo, wali, mkate hukaa tumboni kwa zaidi ya siku tatu, pia unywaji wa vinwaji vitamu vyenyw sukari nyingi unasababisha kuongezeka uzito na pia huongeza ukubwa wa tumbo.

Vyakula hivyo vinatakiwa kutumiwa kwa kiasi kidogo sana. Kuna wakati tumbo linajitokeza na kuwa kubwa kuliko kawaida hali hiyo inasababishwa na kula vyakula vya wanga kwa wingi, kutokunywa maji ya kutosha na pia kula bila ya mpangilio maalum.

Vyakula vya wanga na mafuta hufanya mtu kunenepa, acha au kupunguza kula vyakula hivyo.
Tumbo kuwa kubwa ni dalili kuwa chakula unachokula hakifanyi kazi inayotakiwa, kumekuwa na ziada mwilini na hii ziada inafanya mafuta ambayo hujiwekesha akiba katika maeneo mbalimbali ya mwili.
Kwa kuwa chakula hiki cha ziada huwa hakitakiwi, mwili hukibadilisha na kuweka akiba katika mfumo wa mafuta kitaalam kama glycogem.

Unaweza kukabiliana na kuzidi kwa protini zinazoyeyushwa na kuwekwa katika akiba kwa mfumo huo wa mafuta. Mtu mwenye tatizo hilo ni bora akapangilia mlo wake kwa siku kama ifuatavyo:
Asubuhi pata kifungua kinywa kilichokamilika, pata mlo wa mchana kama kawaida na usiku kula matunda tu kunaweza kufanya mwili wako uwe katika hali inayotakiwa.

Watu wengi wanatumia chakula cha wanga mwingi wakati wa usiku, muda ambao wanakwenda kulala na ziada ya chakula haifanyi kazi vizuri zaidi ya kujikusanya, kujibadilisha na kuhifadhiwa katika maeneo mbalimbali ya mwili hasa tumboni na kwenye makalio.

Mazoezi ya viungo husaidia kuchoma mafuta ya ziada katika mwili. Wanaume huwa na asilimia 8 hadi 20 ya mafuta katika mwili na wanawake ni asilimia 13 hadi 25.
Unapofanya mazoezi ya viungo unaongeza hewa ya oksijeni katika mapafu na wakati huohuo mwili nao unaunguza mafuta ili kutoa nguvu kwa mwili. 
Kwa ushauri zaidi wasiliana na daktari.

Saturday, 9 July 2016

HIVI HAPA VYAKULA 7 VIZURI ZAIDI KWA NGUVU ZA KIUME



Mwanaume mmoja kati ya watatu wana matatizo ya nguvu za kiume – hii ni kulingana na utafiti uliofanyika. Upungufu wa nguvu za kiume unasababishwa na mambo mengi ikiwemo ukosefu wa virutubisho muhimu mwilini. Ni jambo linaloweza kupata ufumbuzi kwa urahisi kama utazingatia kula vizuri na kufanya mazoezi.
Ili kuongeza stamina kwenye mapenzi si lazima kutumia madawa makali kama viagra au vilevi vikali. Madawa na pombe hukupa nguvu zinazoisha kwa muda mfupi, lakini hukuletea madhara makubwa yatakayokuandama kwa muda mrefu zaidi. Ili kupata suluhishi la uhakika ni vizuri kuzingatia vyakula vinavyoweza kukuongezea stamina na kujenga mwili wako vizuri na kukupa uwezo wa kufanya mapenzi vizuri zaidi bila kutumia "booster". Vyakula ni suluhishi maridhawa na asilia kwenye kila kitu maishani mwako.

Sababu za kukosa nguvu za kiume

 Ili kutatua tatizo ni muhimu kung’oa kabisa mzizi wake. Mwili wako una maarifa ya kujirekebisha pasipo kuhitaji vilevi au mawada, unachotakiwa kuzingatia ni chakula bora tu. Wahenga walisema, utakuwa bora kama chakula unachokula. Je wewe unakula chakula bora ili kulinda heshima yako nyumbani?
Vitu vinavyoweza kupelekea kupungua kwa nguvu za kiume ni kama:
  • Kutokuwa na mzunguko mzuri wa damu mwilini, hasa sehemu za viungo vya uzazi kwa mwanaume.
  • Kutokuwa na kiwango cha kutosha cha homoni ya Testosterone
  • Kupungukiwa protini na hivyo kukosa amino asidi mwilini

Jinsi ya kuongeza nguvu za kiume

Leo napenda tuangalie vyakula ambavyo vinasaidia kuboresha nguvu za kiume na kusaidia kwa kiasi kikubwa kudumisha mapenzi na kulinda mahusiano na ndoa.

1. Blueberry

Blueberry ni matunda yanayosaidia sana kuongeza nguvu za kiume, wengi hupendelea kuyaita ‘viagra’ asilia kutokana na kazi inayoifanya mwilini. Blueberries ina virutubishi vinavyoimarisha mishipa ya damu na kusaidia mzunguko mzuri wa damu mwilini. Damu ndio kila kitu katika nguvu za kiume. Vilevile, blueberries zina nyuzinyuzi (fiber) ambazo husaidia kuondoa kolesteroli (Cholestrol) mwilini kabla hazijanganda kwenye mishipa ya damu. Kuwa na mzunguko mzuri wa damu husaidia mwanaume aweze kuhimiri mapenzi wa muda mrefu zaidi.

2. Mtini (Figs)

Mtini (figs) ni matunda yenye kiwango kikubwa cha amino asidi, ambayo ni kiungo kikubwa katika kuzalisha homoni mwilini. Homoni ndio kishawishi cha nguvu za kiume mwilini. Kukosa amino asidi huweza kusababisha kukosa hamu ya mapenzi au kupungukiwa na nguvu za kiume.

3. Chaza/Kombe wabichi (Raw Oysters)

Chaza wana kiwango kikubwa cha madini ya zinc. Madini za zinc hutumika katika utengenezaji wa homoni ya testosterone, shahawa na mbegu za kiume. Uwingi wa uzalishwaji wa testosterone mwilini huathiri pia hamu ya mapenzi na nguvu za kiume – ikiwa kidogo huondoa hamu, ikiwa nyingi hupelekea hamu na nguvu zaidi.
Kupungukiwa kwa madini ya zinc husababisha kupungua kwa nguvu za kiume, udhaifu (uhanithi), na kushuka kwa kiwango cha uwezo wa kufanya mapenzi.

4. Karanga

 
Karanga ni chanzo kikubwa cha kujenga protini mwilini. Karanga huwa na kiwango kikubwa cha amino asidi ambayo husaidia kuweka vizuri mfumo wa damu, hivyo kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha ufanyaji mapenzi.

5. Vitunguu saumu

Kitunguu saumu kina allicin, kiambato kinachosaidia mzunguko mzuri wa damu kwenye viungo vya uzazi. Kuwa na mzunguko mzuri wa damu kwenye uume ni sababu kubwa ya kuongeza stamina ya kufanya mapenzi.

6. Ndizi

Kuwa na stamina ni muhimu katika ufanyaji mapenzi. Ndizi ni chanzo kikubwa cha vitamin B ambayo husaidia sana katika kuongeza stamina na nguvu mwilini hasa wakati wa kufanya kazi nzito. Ndizi ina kimeng’enyo cha Bromelain ambacho huongeza nguvu za kiume, ashki ya mapenzi (libido).

7. Chocolate

Chocolate inasaidia kuongeza stamina kwenye kufanya mapenzi kwasababu ina viambato vya phenylethylamine na alkaloid. Phenylethylamine ni kiambato kinachopelekea kujisikia vizuri, hasa wakati wa kufanya mapenzi na alkaloid huongeza stamina na nguvu wakati wa mapenzi.

Vyakula ni bora kuliko madawa makali

Mie binafsi nashauri kutumia njia asilia katika kutatua matatizo yako yote ya kiafya. Mwili una njia zake za kurekebisha kila kitu. Ukiona kuna tatizo inaashiria kuna upungufu ambao unatakiwa kurekebishwa. Kutumia madawa makali hudhoofisha mwili na hivyo kuupunguzia uwezo wa kufanya kazi kama inavyotakiwa. Ni vizuri kama utamuona daktari kama ukiona hakuna kinachowezekana kabla hujaanza kutumia madawa.
Mara nyingi njia asilia hutumia muda mrefu sana kuleta mabadiliko, lakini matokeo yake hudumu zaidi kuliko kutumia madawa makali ambayo hutibua mfumo wa kawaida wa ufanyaji kazi wa mwili wako. Mie nashauri uangalie jinsi unavyokula, nenda kapime vizuri. Kama jogoo ameshindwa kupanda mtungi, ruksa kuangalia njia mbadala
Ni vizuri kula kwa kiasi kabla ya kufanya mapenzi, hasa wakati wa usiku kabla ya kwenda kulala. Kuvimbiwa husababisha mwili kufanya kazi ya ziada ya kumeng’enya chakula hivyo kuingiwa na uchovu, uvivu na kunyong’onyea. Hii husabisha kukosa usingizi na kupungua kwa umahiri wako katika kufanya shughuli nyingi zinazohitaji nguvu, ikiwemo mapenzi, kwa ufasaha. Usije kumtafuta mchawi wakati wewe ndio unajiroga, kuwa makini.
Kama ilivyo ada kwenye mambo mengi ya kiafya, hakuna muarobaini. Ni vizuri ukajaribu kubadilisha chakula unachokula, fanya mazoezi mara kwa mara ili kupata mwili wenye nguvu. Kama utakuwa na swali, weka maoni hapo chini nasi tutakujibu bila kusika hukusu njia zaidi za kutatua tatizo la nguvu za kiume.

Friday, 8 July 2016

ITAMBUE SIKU YAKO YA UZAZI

SIKU YA UZAZI MZUNGUKO WA KAWAIDA NA MREFU SIKU 28-35

****NOTE, KAMA HUJUI KUHESABU SIKU ZA MZUNGUKO WAKO BASI TAFUTA MAKALA IPO HAPA CHINI
》》》》》

Kwa wale wanandoa wenye uhakika na MIZUNGUKO YAO ya mwezi. Mfano una uhakika kabisa ya kwamba mzunguko wako wa hedhi ni siku 28 au 32 au 35 na kwamba mzunguko huu umeuona kwa muda wa miezi mitatu basi leo nawapa SIRI YENYE UHAKIKA WA 70% kujua siku zako za uzazi.

MZUNGUKO WA SIKU 28 KWA MFANO
SIKU YA 14 NDIO SIKU YA UZAZI.
FORMULA IKO HIVI

>>>>hesabu siku 15 kuanzia siku ya 28 na kurudi nyuma, yaani tarehe 28 siku ya 1, tarehe27 ya pili,26 ya tatu,25 ya nne ,24 ya tano,23 ya sita,22,21,20,19,18,17,16,15, na tarehe 14 ni siku ya kumi na tano

Katika mzunguko huu siku nzuri ya kuanza kuwa karibu na mwenzako ni kuanzia siku ya 12 hadi siku ya 16.

Mfano huu ni kwamba kama umepata bleed tarehe 1 mwezi wa 7 na mzunguko wako ni siku 28 basi tarehe 14 ndio SIKU YA UZAZI, lakini wewe anza shughuli tarehe 12 hadi 16. Hii ni kwa sababu yai likitoka katika nyumba yake ya mayai linaweza ishi masaa24 tu wakati mbegu za kiume zinaweza ishi masaa hadi 72 na zaidi

MZUNGUKO WA SIKU 34 KWA MFANO
SIKU YA 20 NDIO SIKU YA UZAZI
FORMULA IKO HIVI

Hakikisha mzunguko huu ni mzunguko ulioupata katika miezi mitatu iliyopita. Kama mzunguko unarukaruka basi formula hii haiwezi kukufaa.

Mfano Umepata hedhi mwezi wa saba tarehe 1 manayake siku ya 34 ni mwezi wa 8 tarehe 3. Sasa hesabu siku 15 kuanzia tarehe 3 mwezi wa 8 na kurudi nyuma.
Yaani tarehe 3 mwezi wa 8 itakuwa siku ya kwanza ,tarehe 2 mwezi wa 8 itakuwa siku ya 2,tarehe 1 mwezi wa nane itakuwa siku ya 3 ,tarehe 31 mwezi wa 7 itakuwa siku ya 4, tarehe 30 siku ya 5, endelea 29,28,27,26,25,24,23,22,21, hadi tarehe 20 itakuwa siku ya 15.

>>>Katika mfano huu ni kuwa kama umepata bleed tarehe 1 mwezi wa 7 basi SIKU YAKO YA UZAZI ni tarehe 20. Kwa hiyo unatakiwa kuwa karibu na mwenzio kuanzia tarehe 18 hadi 22.

USHAURI WA BURE ni kwamba katika siku hizi Epuka kuwa mgomvi na mnyimi kuwa mkarimu na mpole ili uongeze furaha ya mwenzako afanye kazi kwa bidii na vizuri.

Sasa tarehe zinaambatana pia na dalili moja kubwa ya kuwa na UTEUTE UKENI, ute huu ni ule kama utaingiza vidole viwili katika uke na kisha ukitoa vitanue kama unaweka alama ya V. UTAONA UTE UNAOVUTIKA KAMA UZI.

BASI JUA KWA HAKIKA HIYO NDIYO SIKU YAKO YA UZAZI. Kama utajaribu miezi kadhaa na kukosa kushika mimba basi tambua ya kwamba kuna tatizo lingine kubwa ama kwa mwenzako au kwa wewe mwenyewe.

>>>> IKIWA UNA MATATIZO YA BLEED AU HEDHI YENYE KURUKA RUKA AU HAIPO KABISA AU UNATOA DAMU NYINGI AU INAKAA MUDA MREFU ZAIDI YA SIKU 7 AU NI ILE INATOKA SIKU MOJA TU BASI USISITE KUWASILIANA NASI KWA USHAURI ZAIDI <<<<<

PI UNAKARIBISHWA KUNUNUA PEDI ZETU ZENYE DAWA NA ZENYE UWEZO WA KUTIBU MIWASHO, FANGASI NA MAUMIVU WAKATI WA SIKU ZA HEDHI

Call/txt 0767925000
Watsap 0622925000


Sunday, 22 May 2016

ZIJUE TABIA 10 ZINAZOHARIBU FIGO


By Masha Masanja
Call/txt/whatsapp 0622925000

Kwa kifupi sana leo tunakutajia baadhi ya Tabia zinazochangia kuharibika kwa Figo. Tutambue kuwa tatizo hili la kufeli kwa figo limeshawakumba wengi na baadhi yao wameshapoteza maisha.

Ukiwa mzima mshukuru Mungu na ni vyema ukasoma makala hii ili kujinusuru na janga hili la kuharibikiwa figo.

Hizi hapa ni baadhi ya tabia 10 zinazoharibu figo:
1. Kubana mkojo kwa muda mrefu
2. Kutokunywa maji ya kutosha
3. Kutumia chumvi nyingi
4. Kula nyama mara nyingi zaidi
5. Kutokula chakula cha kutosha
6. Kuchelewa kujitibu maambukizi madogomadogo
7. Kutumia visivyo dawa za maumivu
8. Utumiaji wa madawa kwa ajili ya Insulin
9. Kunywa pombe kupita kiasi
10. Kutopata muda wa kutosha kupumzika


Tafadhari share makala hii kwa watu wengi zaidi ili nao wapate kujifunza na kisha kujinusuru na tatizo hili.



whatsapp 0622925000

Tuesday, 19 April 2016

JINSI YA KUIMARISHA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA KIRUTUBISHO KILICHOTOKANA NA NYANYA



Ni mara nyingi tumekuwa tukizungumza kuhusiana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume chanzo chake pamoja na mambo ya kufanya ili kulimaliza tatizo hilo.

Katika makala zilizopita niliongelea baadhi ya mambo yanayoweza kuchangia kuwa na tatizo hilo. Tembelea www.shinyangabusiness. blogspot.com ili kuyajua mambo hayo ambayo ni pamoja na ulevi, utumiaji wa dawa za kusisimua nguvu za kiume (vega) na upigaji sugu wa punyeto.

Sasa tuone jinsi kirutubisho kilichotengenezwa kutokana na nyanya aina ya Lycopene ambazo hulimwa nchini Thailand kinavyoweza kuwa msaada katika kutibu tatizo hili la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi (mwezi mmoja hadi mitatu).

Kirutubisho hiki ni aina ya nyanya zilimwazo  nchini Thailand ambacho baada ya utafiti wa muda mrefu imedhihirika kuwa kina uwezo mkubwa wa kuboresha uzalishwaji wa mbegu za kiume hivyo kuweza kuwasaidia hata wanaume wenye matatizo ya uzazi au kutozalisha.

Kwa kitendo hicho ina maana kirutubisho hiki kinaimarisha misuli ya uume iliyolegea kutokana na upigaji wa punyeto ambapo ndiyo chanzo kikubwa cha wanaume wengi kuwahi kumaliza (kupizi mapema chini ya dakika 3) wakati wa tendo la ndoa.

Mmea huu wa nyanya sasa umeboreshwa zaidi na unapatikana katika mfumo wa vidonge (capsules) na unaweza kujipatia popote ulipo Tanzania. Maana kama ungebaki katika mfumo wa nyanya ingekuwa ngumu kusafirisha aina hiyo ya nyanya kutoka Thailand hadi barani kwetu Afrika.

Mbali na kusaidia katika masuala ya uzazi, vidonge hivi husaidia pia matatizo mengine kama Presha ya kupanda,  kansa ya matiti,  macho, vidonda vya tumbo, matatizo ya moyo na Asthma.

Kwa wanaume inashauriwa kutumia kirutubisho hiki angalau mara 2 hadi 3 kwa mwaka ili kujikinga na kansa ya TEZI DUME.

Matumizi yake unameza kidonge kimoja asubuhi na jioni pia kimoja.

Waweza jipatia vidonge hivi visivyo na kemikali katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Tanga, Morogoro, Mbeya, Zanzibar na Dar as salaam. Mikoa mingine mnaweza kutumiwa kupitia ofisi za Mabasi

Mawasiliano
0622925000(whatsapp)
0767925000
0784925000


Monday, 11 April 2016

MATIBABU YA MIFUPA, KIUNO, MGONGO NA MACHO YALIYOATHIRIWA NA KISUKARI

KAMA UNA MATATIZO YA MIFUPA, KIUNO, MGONGO, MATATIZO YA MACHO YALIYOATHIRIKA KUTOKANA NA KISUKARI BASI TIBA HII HAPA

Shark cartilage is a dietary supplement made from the dried and powdered cartilage of a shark; that is, from the tough material that composes a shark's skeleton.
Shark cartilage (tough elastic tissue that provides support, much as bone does) used for medicine comes primarily from sharks caught in the Pacific Ocean. Several types of extracts are made from shark cartilage including squalamine lactate, AE-941, and U-995.

Shark cartilage is most famously used for cancer, including a type of cancer called Kaposi’s sarcoma, that is more common in people with HIV infection. Shark cartilage is also used for arthritis, psoriasis, wound healing, damage to the retina of the eye due to diabetes, and inflammation of the intestine (enteritis).

Some people apply shark cartilage directly to the skin for arthritis and psoriasis.

FOR MORE DETAILS PLEASE CALL US ON 0767925000 OR WHATSAPP 0622925000.

TUTAKUTUMIA POPOTE ULIPO...!


Friday, 8 April 2016

ANGALIA VYAKULA HIVI VINAVYOIMARISHA VIUNGO VYA UZAZI VYA MWANAUME

VYAKULA HIVI VI 4 VITAKUSAIDIA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME.
Kichocheo cha testosterone au kwa Kiswahili , japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume.
.KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA, KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI.
NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE?
Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhiwakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wetu tunakosa vitamini D kwa sababu muda mwingi tunautumia tukiwa ndani tukiendelea na shughuli zetu. Zinc ni madini muhimu ambayo hupatikana kwenye baadhi ya vyakula.

NINI HASA KINASABABISHA KUPUNGUA KWA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE KWENYE DAMU
Mawazo au stress ni muuaji asili wa kichocheo cha testerone, pale unapokuwa na stress basi Tezi ya Adrenal hutengeneza kichocheo iitwayo Cortisol ambayo inapoenda kwenye damu hupunguza ufanyaji kazi wa kichocheo cha kiume cha testosterone ndani ya mwili. Hivyo kama unataka kuepusha tatizo hili ni wazi kwamba unahitaji kupuza stress na kiwango cha cortisol.

AINA ZA VYAKULA AMBAVYO HUSAIDIA KUONGEZA UZALISHAJI WA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE
Ijapokuwa kuna njia nyingi za kusaidia kuongeza kiwango cha kichocheo cha kiume au Testosterone, uzalishaji wa kichocheo hii unategemea zaidi upatikanaji wa viini lishe fulani ambavyo vinapatikana ndani ya vyakula tunavyotumia.

1. KOMAMANGA (POMEGRANATE)
Tunda hili zuri lenye rangi nyekundu likiwa limeiva limekuwa likitumika kama dawa kwa karne nyingi sasa. Kutokana na uwezo wake mkubwa kama kiondoa sumu (antioxidant), pia upatikanaji wa vitamini A,C, E na madini ya chuma, tafiti za kisayansi zinasema kuwa unywaji wa glass 1 ya juisi kwa siku itokanayo na matunda haya inaongeza kwa asilimia 16 mpaka 30 ya hamasa ya tendo la ndoa. Lakini pia inashauriwa zaidi kula tunda lenyewe ili kwanza kufaidi nyuzinyuzi (fiber) ambazo zina umuhimu kiafya pia itakusaidia kutokula kiwango kikubwa cha sukari kilichopo kwenye matunda.

2. MAFUTA YA MIZEITUNI
Mafuta ya mizeituni yana uwezo mkubwa sana wa kuongeza kiwango cha kichocheo cha Testesterone kinachozalishwa na mwili. Tafiti zinasema watu wanaotumia mafuta ya mizeituni kila siku,kiwango cha testosterone huongezeka kwa asilimia 17 mpaka 19 ndani ya week.

3. NAZI
Mwili unahitaji mafuta mazuri ili kuengeneza kichocheo nyingi, ikiwemo kichocheo cha testosterone. Nazi zinasaidia mwili kutengeneza mafuta mazuri ambayo yanahitajika na mwili, pia mafuta yanayopatikana kwenye nazi husaidia mwili kuwa na uzito mzuri na pia kupunguza mafuta mabaya yasiyohitajika na mwili na hivyo utagundua kuwa kurekebishwa kwa uzito wa mwili basi kunasaidia uzalishaji wa kichocheo cha kiume na utakubaliana nami kuwa uzito mkubwa ni chanzo cha tatzo la upungufu wa nguvu za kiume kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa kichocheo cha kiume.

4. MBOGA ZA MAJANI
Mboga za broccoli na cauliflower zinasaidia mwili wa binadamu kutoa kiwango cha kichocheo cha estrogen kilichozidi ndani ya mwili na hivyo kuongeza kiwango cha testosterone ndani ya seli

5. PROTINI ITOKANAYO NA MAZIWA
Protini hii ambayo hupatikana kwenye sehem ya maji ya maziwa inazuia mwili kutengeneza kias kikukwa cha kichocheo cha cortisol na hivyo kuongeza uzalishwaji  na ufanyaji kazi wa wa kichocheo cha  Testosterone, hapa ielewele kwamba kichocheo hizi mbili huwa zinapishana moja ikiwa nyingi kwenye damu basi ingine huwepo kwa kias kidogo kwenye damu.

DALILI ZIFUATAZO ZINAONESHA KWAMBA UNA UPUNGUFU WA KIWANGO CHA TESTOSTERONE
• Mwili kukosa nguvu mara kwa mara
• Upungufu wa nguvu za kiume
• Kupungua kwa hamasa ya tendo la ndoa
• Kuongezeka uzito kupita kiasi
• Shinikizo la damu kupanda
• Kupungua kwa uwezo wa misuli kufanya kazi

NJIA ZIFUATAZO ZITASAIDIA KUONGEZA KIWANGO CHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE
1. MAZOEZI YA MWILI
Kupunguza uzito usiohitajika na mwili ni njia mojawapo asilia ya kuongeza kiwango cha kichocheo cha kiume.

2. PUNGUZA KIWANGO CHA MSONGO WA MAWAZO
Mwili Unapokuwa na msongo wa mawazo basi hupelekea uzalishaji kwa wingi wa homoni iitwayo cortsol ili kupamban na hali hiyo, lakini uoande wa pili ni kwamba kiwango kikubwa cha cortsol kwenye damu hupelekea ufanyaji kazi ya homoni ya kiume yaani testosterone kupungua

3. PUNGUZA MATUMIZI MAKUBWA YA VYAKULA VYENYE SUKARI NA WANGA
Matumizi makubwa ya vyakula vyenye wanga na sukari hupelekea mwili kutengezeza kiwango kikubwa cha homoni ya insuini ili kubadilisha kiwango hcho cha sukari na kukihifadhi kama mafuta, hivo mpenzi msomaji tambua kwamba kadiri unakula wanga na sukari nyingi ndipo kias kikubwa cha insulini kinavomwagwa kwenye damu na ndivyo ufanini na utolewaji wa homoni ya kiume unavopungua.

TEZI DUME NI NINI?? Na UHUSIANO ULIOPO KATI YA TEZI DUME NA UZALISHAJI WA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE
TEZI DUME NI NINI
Hii ni tezi (kokwa) ambayo inapatikana katika mfumo wa uzazi wa mwanaume katika shingo ya kibofu cha mkojo. Kazi yake kubwa ni kutengeneza maji maji ya uzazi kwa mwanaume(shahawa) ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizotengenezwa kutoka kwenye korodani na husaidia kusafirisha mbegu za kiume na kuzifanya zibaki hai kwa muda unaostahili. Kikawaida wanawake wana kiwango kidogo sana cha kichocheo cha testosterone kwa maisha yao yote
Tezi hii huwa inaongezeka uzito au ukubwa kadri umri wako unavyozidi kukua. Na nimekwambia kuwa tezi hii ipo katika shingo ya kibofu cha mkojo na hivyo basi ukuaji wake unaweza kuathiri mfumo mzima wa utoaji mkojo kwenye kibofu(Incomplete bladder emptying) .

Tafiti zinaonesha kwamba tezi huanza kuongezeka uzito kuanzia miaka 25, na huendelea kukua kila siku kadri umri unavyo enda. Kuongezeka kwa uzito wa tezi yako ya kiume sio tatizo kimatibabu kwani kipimo cha kuonesha moja kwa moja umefikia hatua sio nzuri ni pale unapoanza kupata dalili zenye kuzuia mkojo kutotoka vizuri (obstructive symptoms). Hivyo uzuri ni kwamba kuanzia pale tezi inapokuwa inaongezeka ukubwa hadi kufikia kuonesha dalili mbaya ni hadi unapofikia angalau umri wa miaka 60 na kuendelea , pia inaweza hata ikatokea hata unapokuwa una umri chini ya miaka 50 inategemea na mwili wako kibaolojia. Basi kukua huku kwa tezi bila sababu ya msingi tunaweza tukawa na hitimisho la magonjwa makuu mawili au matatu,Kwanza Benign Prostate Hypertrophy (BPH) aka Kukua kwa tezi dume, pili Prostate cancer Hii ni kansa ya tezi dume na Tatu Uvimbe kwenye kibofu cha mkojo.

Tafiti zinasema kwamba tatzo la Tezi dume linaweza kuziwa kutokea kwa njia za nje, yaani namnisha kwa kutumia ama kula vyakula fulani fulani, kiwango kikubwa cha kiini lishe kiitwacho lycopene husaidia kuondoa uwezekano wa mtu kuugua tezi dume. Lycopene hupatina akwenye matunda yanya. Hapa mpenzi msomaji unaweza kujiuliza kama tunatumia nyanya kila siku kwenye mboga je iweje tuugue tatizo la tezi dume?? Jibu ni kwamba kiasi kidogo sana  cha lycopene hufonzwa na mwili kutoka kwenye matunda ya nyanya tunayokula hivo inahitaji ule mamia ya nyanya kila siku ili kufidia hilo gepu.

LAKINI KAMA TAYARI UMESHAPATA TATZO LA KUKUA KWA TEZI DUME BASI TUMEFANIKIWA KUTENGENEZA KIRUTUBISHO KUTOKANA NA NYANYA, kitasaidia kupenya ndani ya tezi dume, kuua bacteria na pia kukarabati sehem zilizoathiriwa na bacteria na hivyo kuzuia kutokea kwa saratani ya tezi dume.

Kirutubisho hiki  kina vidonge 30 na unatumia vidonge viwili mara mbili kwa siku. Kwa maoni ushauri na tiba tunapatikana whatsapp/text no 0622925000

Usisahau kushare makala hii kwa ndugu marafiki na jamaa zako.

Masha Masanja


Thursday, 31 March 2016

JINSI YA KUTAMBUA KAMA UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILI WAKO


By: Masha Masanja
Call/txt/whatsapp 0622925000
Email: mashamasanja@gmail.com

Watu wengi tumekuwa tukiishi kwa kutojua miili yetu kama ipo sawa, hii ni kutokana na kile kitendo pengine cha kutougua hutufanya tujisahau kabisa katika kujua undani wa Afya yetu.

Leo napenda tujifunze namna ya kujua jinsi gani utatambua kuwa UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILI WAKO(BODY MASS INDEX kwa kifupi BMI)

Kwa kifupi kitendo hiki huhusisha vitu viwili ambavyo ni uzito wako katika kilogram(kg) pamoja na urefu wako katika mita(m). Tutajifunza kwa kutumia mfano.

Uhusiano huo upo katika mpangilio kama ifuatavyo:
BMI ikiwa chini ya 18.50 hapa inakuwa mtu huyu uzito wake upo chini kuliko kawaida(UNDER WEIGHT)

BMI kuanzia 18.50 hadi 24.99 huyu mtu ni mwenye Afya njema na yuko vizuri kabisa(HEALTHY)

BMI kuanzia 25.00 hadi 29.99 huyu ni mtu ambaye amezidi uzito(OVER WEIGHT) hivyo uzito wake na urefu wake haviendani kabisa.

BMI kuanzia 30.00 na kuendelea basi huyu mtu ni yule aliyepitiliza kabisa kiwango cha uzito na anaingia katika kundi la Obesity.

Sasa unapata vipi uhusiano wa uzito na urefu wako(BMI)?

Angalia hapa chini

Kanuni(BMI)=uzito ÷ (urefu)kipeo cha pili
      
Tuangalie mfano mimi Masha nina uzito wa kg 64 na urefu wa sentimeta 162 ambao ni sawa na mita 1.62

BMI ya Masha=64/1.62×1.62
BMI=64/2.6244
BMI=24.386

Kwa mfano huo basi Masha yupo kwenye kundi salama japo bado kidogo tu afikie 25 ambapo siyo pazuri.

Sasa tufanye ya kwamba Masha ana uzito wa kilo 74 na urefu uleule

BMI= 74/2.6244
BMI=28.196
Hapa anakuwa OVER WEIGHT

Na endapo Masha ana uzito wa kg 91;
BMI=91/2.6244
BMI=34.6745
Hapa ni OBESITY!!

Ndugu msomaji wa makala hii nadhani sasa umeshafahamu namna ya kujua kama una uzito unaoendana na urefu wako, hivyo unaweza kujifanyia tathimini wewe mwenyewe.

NOTE: UREFU WAKO UWE KATIKA KIPIMO CHA MITA(METRE).

Unaweza ku-share zaidi makala hii kwa watu wengi kadri uwezavyo ili nao waweze kujifunza kama ulivyojifunza wewe.

Pia huwa ninatoa ushauri na mafunzo maalumu jinsi ya kupunguza uzito/kitambi na nyamazembe kwa kutumia chakula tu, chakula hicho kitaubadili mwili  uwe mashine ya kuunguza mafuta.

Wednesday, 30 March 2016

Hebu angalia faida 50 za kufanya mazoezi ya viungo ndani ya mwili wako

Umuhimu wa mazoezi kwa afya bora na maisha marefu bila maumivu.

Moja ya mahitaji matano (5) mhimu ili kuishi baada ya oksijeni, maji, chumvi, na potasiamu; ni Mazoezi. Mazoezi ni muhimu kwa ajili ya afya zaidi ya kuwa na maumbile ya kuvutia (sex body), burudani au kitu kingine chochote.

Watu wengi hufuatilia kuhusu chakula tu, hata kama utakula vizuri vipi bila mazoezi mlo haujakamilika, kwa hiyo mazoezi ni mhimu kwa yeyote kama ilivyo kwa maji au chakula.
Hizi ndizo faida 50 za mazoezi

Zifuatazo ni moja ya sababu 50 mhimu za kufanya mazoezi kwa afya bora na maisha marefu bila maumivu:

1. Hukufanya ujisikie vizuri
2. Huongeza uwezo wa kujifunza
3. Hujenga uwezo wa kujistahi
4. Huongeza nguvu ya ubongo kufanya kazi
5. Huuweka mwili wako kuwa unaofaa (fit) na wenye uwezo
6. Huongeza afya ya akili yako
7. Huongeza kinga ya mwili
8. Hupunguza mfadhaiko/stress
9. Hukufanya ujisikie vizuri/mwenye furaha
10. Hukufanya usizeeke mapema
11. Huweka ngozi yenye mng’aro na yenye afya
12. Husaidia kupata usingizi mtulivu
13. Husaidia kuzuia ugonjwa wa kiharusi/strokes
14. Huongeza ufanisi katika makutano/joints za mwili
15. Huongeza nguvu za mishipa
16. Huondoa wasiwasi
17. Huongeza kumbukumbu
18. Husaidia kudhibiti ulevi/uteja
19. Huongeza uzalishaji
20. Huongeza uwezo wa ubunifu
21. Hupendezesha muonekano wa mwili
22. Huongeza uwezo wa kujiamini
23. Husaidia kuongeza nguvu juu ya malengo yako maishani
24. Huondoa tatizo la kukinaishwa na chakula
25. Huongeza miaka ya kuishi
26. Hukomaza mifupa
27. Huongeza afya ya moyo
28. Huongeza hali ya kuwa na msimamo
29. Huondoa homa ndogo ndogo mwilini
30. Huongeza hamu ya kula
31. Hudhibiti usawa wa lehemu/kolesteroli
32. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na baadhi ya kansa
33. Hushusha shinikizo la juu la damu/BP
34. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na kisukari
35. Huzuia kupatwa na ukichaa/uwendawazimu
36. Hupunguza au huzuia maumivu ya mgongo
37. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa mifupa
38. Hupunguza hisia/fikra za kujisikia vibaya au kupiga punyeto kwa vijana
39. Huzuia kupotea kwa mishipa
40. Huongeza nguvu na ustahimilivu
41. Huongeza ufanisi katika michezo
42. Huongeza uwezo wa kuvumilia maumivu
43. Huongeza usawa na ushirikiano wa mwili
44. Huongeza usambazaji wa oksijeni katika seli za mwili
45. Huongeza hali ya ufuatiliaji/concentration
46. Huongeza uwezo wa kujitawala na kujidhibiti nafsi
47. Huondoa uchovu
48. Huongeza nguvu katika tendo la ndoa
49. Hufanya maisha kuwa yenye kuvutia zaidi
50. Huongeza ubora wa maisha

Mazoezi yafuatayo ni mazuri sababu ya thamani yake ya baadaye na hayasababishi maumivu kwenye maungio, nayo ni; kutembea kwa miguu, kuogelea, kuendesha baiskeli, kucheza tenisi, gofu, kukwea, kuruka kamba, kudansi na kadhalika.


Tafadhari share makala hii ili na wengine wajifunze kama wewe

Naitwa Masha Masanja, mshauri wa Afya. Pia ninatoa program maalumu kwa mtu anayehitaji kupungua uzito/kitambi au nyamazembe.

Mawasiliano:
0622925000 - whatsapp
0767925000
0784925000